BANDA MEDIA BLOG

MAZOEA KWA WAUMINI YAKWAMISHA MIUJIZA MAKANISANI

 

Apostle Silas akifafanua jambo wakati alipokuwa akihubiri kwenye kanisa la Living Water Internatiaonal Ministries lililopo chinyoya jijini Dodoma

Prophet Peter GM. wa kanisa la Living Water Internatiaonal Ministries lililopo chinyoya jijini Dodoma akifanya maombizi maalum kwa wenye mahitaji mbalimbali, mara baada ya ibada ya jumapili januari 25,2026

                                                  .............................

Na John Israel, Banda Media Dodoma

PAMOJA na uwepo wa madhabahu nyingi za maombi na maombezi lakini wahusika wamekuwa hawapokei miujiza kutokana na Roho ya Mazoea iliyowakumba waumini wanaosali katika madhabahu hizo.

Kauli hiyo Nzito imetolewa na Mchungaji Silas wa Madhabahu ya Pembe 7 za Mungu iliyopo Njilo Jijini Arusha, wakati alipokuwa akihubiri katika Ibada ya Jumapili januari 25,2026 katika kanisa la Living Woter Internationa Ministries lililopo Chinyoya jijini Dodoma

Mchungaji huyo amesema, Roho ya mazoea imewasababishia wengi kushindwa kupokea miujiza yao wanapoombewa, huku Roho hiyo ikiwasababishia hata kutohudhulia ibada kwa uaminifu.

“watu wanacheza na madhabahu, imefika wakati mtumishi anaweza kumuombea mtu kwa style yoyote na mtu huyo asipokee muujiza wake, kwa sababu ya roho ya mazoea iliyovaa baadhi ya waumini,

hatuji kanisani kwa ajili ya kuja kujaza viti au kujionyesha bali tunakuja kupokea, na ili upokee inategemea na jinsi ulivyojiandaa”, amesema na kuongeza

Prophet Peter GM. wa kanisa la Living Water Internatiaonal Ministries lililopo chinyoya jijini Dodoma akifanya maombizi maalum kwa wenye mahitaji mbalimbali, mara baada ya ibada ya jumapili januari 25,2026

Aidha amesema kila mtu anayo haki ya kupokea kinachotolewa, na watumishi madhabahuni isipokuwa tatizo la walio wengi ni Kiburi.

Ameongeza kuwa kwa upande wa watumiaji wa madhabahu ya Living Water, wakiwemo waimbaji wa kwaya, kusifu na Kuabudu, wahakikishe wanautunza utakatifu ambao kwa mwaka huu ndiyo msimamo wa kanisa hilo.

“waimbaji ninyi ni lango la sifa ambapo Mungu hupishia kwenu hivyo hakikisheni manautunza utakatifu, najua wengi wenu mnafanya makosa, niwaonye kuwa kila mtu anayeitumia madhabahu hii kuhakikisha mnabadilika ili tumrahisishie Mchungaji wetu Peter GM kazi’’,

Prophet Peter GM. wa kanisa la Living Water Internatiaonal Ministries lililopo chinyoya jijini Dodoma akiongea jambo kwenye ibada hiyo ya iliyofanyika januari 25,2026

Prophet Peter GM. wa kanisa la Living Water Internatiaonal Ministries lililopo chinyoya jijini Dodoma, akiwa pamoja na Mgeni wake Apostle Silas kutoka Madhabahu ya Pembe 7 za Mungu lililopo, Njilo jijini Arusha wakiongoza maombizi maalum kwa wenye mahitaji mbalimbali, kwenye ibada ya jumapili januari 25,2026

Post a Comment

Previous Post Next Post
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG