Prophet Peter GM. wa kanisa la Living Water Internatiaonal Ministries lililopo chinyoya jijini Dodoma akifanya maombizi maalum kwa wenye mahitaji mbalimbali, mara baada ya ibada ya jumapili januari 25,2026
.............................
Na John Israel, Banda Media Dodoma
PAMOJA na uwepo wa madhabahu nyingi za maombi na
maombezi lakini wahusika wamekuwa hawapokei miujiza kutokana na Roho ya Mazoea
iliyowakumba waumini wanaosali katika madhabahu hizo.
Kauli hiyo Nzito imetolewa na Mchungaji Silas wa
Madhabahu ya Pembe 7 za Mungu iliyopo Njilo Jijini Arusha, wakati alipokuwa
akihubiri katika Ibada ya Jumapili januari 25,2026 katika kanisa la Living
Woter Internationa Ministries lililopo Chinyoya jijini Dodoma
Mchungaji huyo amesema, Roho ya mazoea
imewasababishia wengi kushindwa kupokea miujiza yao wanapoombewa, huku Roho
hiyo ikiwasababishia hata kutohudhulia ibada kwa uaminifu.
“watu wanacheza na madhabahu, imefika wakati mtumishi
anaweza kumuombea mtu kwa style yoyote na mtu huyo asipokee muujiza wake, kwa
sababu ya roho ya mazoea iliyovaa baadhi ya waumini,
hatuji kanisani kwa ajili ya kuja kujaza viti au
kujionyesha bali tunakuja kupokea, na ili upokee inategemea na jinsi
ulivyojiandaa”, amesema na kuongeza
Prophet Peter GM. wa kanisa la Living Water Internatiaonal Ministries lililopo chinyoya jijini Dodoma akifanya maombizi maalum kwa wenye mahitaji mbalimbali, mara baada ya ibada ya jumapili januari 25,2026
Aidha amesema kila mtu anayo haki ya kupokea
kinachotolewa, na watumishi madhabahuni isipokuwa tatizo la walio wengi ni
Kiburi.
Ameongeza kuwa kwa upande wa watumiaji wa madhabahu
ya Living Water, wakiwemo waimbaji wa kwaya, kusifu na Kuabudu, wahakikishe
wanautunza utakatifu ambao kwa mwaka huu ndiyo msimamo wa kanisa hilo.
“waimbaji ninyi ni lango la sifa ambapo Mungu hupishia
kwenu hivyo hakikisheni manautunza utakatifu, najua wengi wenu mnafanya makosa,
niwaonye kuwa kila mtu anayeitumia madhabahu hii kuhakikisha mnabadilika ili
tumrahisishie Mchungaji wetu Peter GM kazi’’,
Prophet Peter GM. wa kanisa la Living Water Internatiaonal Ministries lililopo chinyoya jijini Dodoma akiongea jambo kwenye ibada hiyo ya iliyofanyika januari 25,2026
Prophet Peter GM. wa kanisa la Living Water Internatiaonal Ministries lililopo chinyoya jijini Dodoma, akiwa pamoja na Mgeni wake Apostle Silas kutoka Madhabahu ya Pembe 7 za Mungu lililopo, Njilo jijini Arusha wakiongoza maombizi maalum kwa wenye mahitaji mbalimbali, kwenye ibada ya jumapili januari 25,2026