BANDA MEDIA BLOG

MCHANGA WA MAAJABU UPO NGORONGORO UNAJITENGENEZA NUSU MWEZI KISHA UNAHAMA (SHIFTING SANDS)

 


Waswahili husema tembea uone na Mwenda bure si mkaa bure huenda ataokota.

Ukitaka kujaribu kuuokota mchanga unaohama njoo jirani na bonde la Olduvai ndani ya hifadhi ya Ngorongoro ushangae, badala ya kubaki ukishangaa maji yanavyokupwa na kujaa Bahari ya hindi na huko Ziwa nyasa na Victoria

Jirani na bonde hili la Olduvai kuna mchanga unaohama ambao huwavutia mealfu ya watalii kuja kujionea maajabu hayo.

Mchanga huu upo katika umbo la nusu mwezi na upo karibu na Bonde la Olduvai ndani ya Hifadhi ya Ngorongoro. 

Mchanga huu wenye rangi nyeusi umetokana na madini ya chuma na majivu yaliyotokana na mlipuko wa Volcano kutoka Mlima Oldoinyo Lengai.

Mchanga huu ambao husogea kwa kasi ya takribani mita 15–29 kwa mwaka tuta lake lina urefu wa mita 5 na upana wa mita 100.

Hayo ndiyo maajabu ya Hifadhi ya Ngorongoro ukitaka kujua zaidi kuhusu mchanga huu tembea uone kwani fahari ya macho ni kuona na fahari ya macho haifilisi duka.

 _Tumerithishwa, Tuwarithishe_

Post a Comment

Previous Post Next Post
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG