
Msigwa ametoa kauli hiyo Jumamosi Januari 10, 2026, wakati wa hafla ya Rais Samia Suluhu Hassan ya kuipongeza timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars, pamoja na wanamichezo wengine inayofanyika Ikulu jijini Dar es Salaam.
“Huyu ni Sanjenti wa KMKM, alimkaba yule Osimhen anayecheza Galatasary mpaka akakasirika akatolewa na hakufunga na Bacca amekuwa maarufu dunia nzima,” amesema.
Hafla hiyo ilihudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Serikali, viongozi wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), benchi la ufundi, wachezaji wa Taifa Stars pamoja na wadau wa michezo
Tags
HABARI/ MICHEZO