BANDA MEDIA BLOG

SMZ YAAHIDI USHIRIKIANO NA VYAMA VYA USHIRIKA KUINUA UCHUMI WA VIJANA

 

                                               Rahma Khamis Maelezo. 

Naibu Waziri wa Vijana, Ajira na Uwezeshaji Mhe Hassan Khamis Hafidh amesema Serikali ya Awamu ya nane ipo tayari kushirikiana na vyama vya ushirika ili kuwainua kiuchumi

Ameyasema hayo katika Ukumbi wa Umoja wa Washirika wa Uchukuzi Bandarini Wilaya ya Mjini katika ziara kutembela Taasisi zilizomo katika Wizara yake na kujitambulisha 

Amesema kuwa vyama vya Ushirika vina Mchango mkubwa katika kukuza Uchumi hivyo Serikali itaunga mkono juhudi zinazofanywa na vyama hivyo ili kufikia lengo lililokusudiwa

Amesema kuwa Kuwepo wa vyama hivyo kunasaidia kujikomboa kiuchumi na kuinua kipato Cha mtu mmoja mmoja na Taifa kwa ujumla

Naibu Waziri amefahamisha kuwa Serikali ina jukumu la kuhakikisha vyama vya ushirika vinafanya kazi kwa kufuata taratibu ili kuondoa umasikini 

Aidha amevitaka vyama hivyo kuacha kulumbana na badala yake kushirikiana katika kazi kwa maslahi yao sambamba na kuwekeza katika taasisi ili kufikia malengo

Mwenyekiti wa Umoja wa Ushirika wa Wachukuzi Bandarini (UWABAZA) Masuod Haji Juma ameiomba a Wizara kupatiwa elimu ya utunzaji wa Fedha kwa wahasibu kwani wanahitaji uwazi katika ukusanyaji wa mapato 

Wakitoa malalamiko yao wanachama wa vyama hivyo wameomba kupatiwa malipo kwa wakati ili kujikimu kimaisha na kuondosha malalamiko kwa baadhi ya wafanyakazi

Katika ziara hiyo Naibu Hafidh ameltembelea vyama mbalimbali vya Ushirika ikiwemo Sacoss zote bandarini,Boat Boys Syndicate Bandarini, Tax Service Bandarini,Tax Saccos Office na Muungano wa Umoja wa vyama vya Ushirika Kikwajuni.

   

Post a Comment

Previous Post Next Post
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG