Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Msalato kukamilika Juni, 2026
Moshi mweupe wa matumaini umeanza kufuka Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Msalato Jijini Dodoma baada ya Waziri wa Uchukuzi Prof. Makame Mbarawa kueleza kuwa ndege zitaanza kuruka na kutua kuanzia Juni mwaka huu.
Uwanja huo kwa sasa umefikia asilimia 75.9, ukihusisha kazi mbalimbali ikiwemo barabara ya kuruka na kutua ndege. Kazi hiyo imefikia asilimia 99 na jengo la abiria limefikia asilimia 99.
Aidha, wakazi wanaozunguka mradi huo wameipongeza Serikali kwa kuendelea kutoa fedha kukamilisha mradi huo na wananufaika na fursa mbalimbali ikwemo ajira.
Tags
HABARI KITAIFA



