Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba akiweka jiwe la msingi la Ujenzi wa Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Kiteto mkoani Manyara leo tarehe 26 Februari, 2026. Ofisi hiyo itagharimu kliasi cha Shilingi bilioni 1.85 hadi kukamilika kwake ambapo hadi sasa ujenzi umefikia asilimia 85. PICHA NA OFISI YA WAZIRI MKUU
Muonekano wa Jengo la Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Kiteto mkoani Manyara ambayo Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Ncheba leo tarehe 26 Februari, 2026 ameweka jiwe la msingi. Ofisi hiyo itagharimu kliasi cha Shilingi bilioni 1.85 hadi kukamilika kwake ambapo hadi sasa ujenzi umefikia asilimia 85. PICHA NA OFISI YA WAZIRI MKUU
Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba akizungumza na wananchi mara baada ya kuweka jiwe la msingi la Ujenzi wa Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Kiteto mkoani Manyara leo tarehe 26 Februari, 2026. Ofisi hiyo itagharimu kliasi cha Shilingi bilioni 1.85 hadi kukamilika kwake ambapo hadi sasa ujenzi umefikia asilimia 85. PICHA NA OFISI YA WAZIRI MKUU
Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba akivishwa vazi rasmi la kiutamaduni wa kimasai ikiwa ni ishara ya kumvika hadhi ya kiuongozi wa kimaasai leo tarehe 26 Februari, 2026 wakati akikaribishwa kwa ziara zake za kikazi Kiteko mkoani Manyara. PICHA NA OFISI YA WAZIRI MKUU
……
WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba, amemtaka Kamanda wa TAKUKURU Mkoa wa Manyara, Bahati Haule, kufanya uchunguzi wa kina na kuwasilisha taarifa ya kila mmoja aliyehusika kuchukua fedha za mradi wa ujenzi wa Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Kiteto.
Mheshimiwa Dkt. Mwigulu amesema kuwa pamoja na kurejeshwa kwa fedha hizo, ni lazima hatua za kinidhamu zichukuliwe dhidi ya watumishi wote waliohusika na mpango huo ili kuimarisha uwajibikaji katika usimamizi wa rasilimali za umma.
Amesema hayo leo Alhamisi (Februari 26, 2026) baada ya kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Kiteto. Ofisi hiyo itagharimu kiasi cha shilingi bilioni 1.85 hadi kukamilika kwake, na ujenzi wake umefikia asilimia 85.
“Kamanda wa TAKUKURU, ninataka uniletee taarifa hii kabla sijamaliza ziara yangu katika Mkoa wa Manyara. Ninahitaji taarifa za mtu mmoja mmoja kwa wote waliohusika kuchukua fedha hizo. Hatukutumwa kuja kuchukua fedha za umma, hatua za kinidhamu lazima zichukuliwe,” amesisitiza.
Kadhalika, Mheshimiwa Dkt. Mwigulu amesema kuwa mbali na taarifa hiyo, anataka pia kuwasilishwa taarifa za mapato ya ndani, ikiwemo mapato yatokanayo na minada, zikionyesha namna yanavyokusanywa na kutumika. “Hakuna kuvumilia ubadhirifu wa mali ya umma. Tunataka kila mtu aheshimu fedha za utekelezaji wa miradi,” amesema.
Katika hatua nyingine, Mheshimiwa Dkt. Mwigulu amesema kuwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ana dhamira ya dhati ya kutatua changamoto za Watanzania, akisisitiza kuwa lengo lake ni kuona maendeleo endelevu yanapatikana nchini
