BANDA MEDIA BLOG

MKUTANO WA VIONGOZI WA IRAN KUSHAMBULIWA NI WAIRAN KUDOKOA MBOGA AU C.I.A

 


JE C.I.A. Ilisaidia Kubaini Mkutano wa Viongozi wa Iran, kisha Israel Ikashambulia,? au Wairan wasio watiifu walidokoa mboga?

Kuuliwa kwa kiongozi mkuu wa Iran na maafisa wengine wa juu wa Iran kulitokea baada ya ushirikiano wa karibu wa kijasusi kati ya Marekani na Israel, kwa mujibu wa watu wanaofahamu operesheni hiyo.
Watu wanaofahamu operation hiyo ni kina nani??
Hebu turudi katika nukuu za siku za nyuma........................
CNN Türk
Katika mahojiano ya kusisimua na CNN Türk, rais wa zamani wa Iran, Mahmoud Ahmadinejad, alidai kwamba kitengo kilichoundwa cha Huduma ya Siri ya Iran kushughulikia maajenti wa Mossad kilikuwa kimeingiliwa sana na Ujasusi wa Israel.
Eeheee !!
Kiongozi wa ngazi ya juu aliyepewa jukumu la kuongoza kitengo cha kupambana na Mossad alikuwa ajenti wa pande mbili, mwenyewe akiwa ni mjasusi wa Israel.
Hadithi njoo!!
Pamoja na kiongozi huyo, angalau maajenti 20 wengine katika kitengo hicho walikuwa wakifanya kazi kama maajenti wa pande mbili kwa Israel.
Endelea!!
Ahmadinejad alihusisha kikundi hiki na uvunjaji wa usalama wa hali ya juu, ikiwemo:
kuibwa kwa kumbukumbu kubwa za nyaraka za nyuklia za Iran mwaka 2018.
Mauaji yaliyolengwa ya wanasayansi wa nyuklia wa Iran.
Rais huyo wa zamani alisema kwamba ingawa kiongozi wa kitengo kiligunduliwa mwaka 2021, wengi wa maajenti hawa waliweza kukimbia Iran na kwa sasa wanaishi Israel.
Alaah kumbe
Idara ya Ujasusi (MOIS) nchini Iran ni Idara yenye utendaji wa hali ya chini sana naweza kusema ni idara ya hovyo kabisa kiutendaji.
Intellijensia nzima ya Iran ina kasoro kubwa kiasi kwamba mtu unaweza kushawishika kusema kuwa pengine kuna watu ndani humo humo ya idara pengine wanafanya kazi moja kwa moja na Marekani na Israel.
Nimeshangaa! Unaweza vipi kuruhusu kiongozi wako mkuu wa nchi tena mtu pekee anayetafutwa kufanya kikao kwenye eneo la ofisi yake sehemu ambayo inajulikana kwa kiasi kikubwa kwamba ni Ofisi ya Kiongozi mkuu wa kiimani wa Iran.
Nimeshangaa! Ndege za Marekani na Israel zimepita katika nchi kadhaa hadi kufika nchini Iran unataka kuniambia katika nchi zote hizo Iran hakuwa na watu wake wakuripoti mara moja uelekeo wa ndege hizo.
Wote tunakubaliana kuwa Iran ana makombora mengi tu ya kisasa ila shida huwezi kupigana vita bila kuwa na Intellijensia bora ambayo itakupa uwezo wa kujilinda na kujiweka sawa kama adui akianzisha mashamnulizi dhidi yako.
Vita ni mkakati, Iran hakuwa na mkakati wowote hakufahamu wapi ashambulie pindi akishambuliwa, kiufupi hakujiandaa na mkakati wowote wa kivita.
Marekani na Israel wamewekeza kwa kiasi kikubwa sana katika Intellijensia na ndio maana unaona kuna majasusi kibao wa CIA na MOSSAD nchini Iran, hawa kazi yao kubwa ni kuangalia nyendo nzima za watu wao wanaowatafuta.
Sasa tuendelee na habari
Muda mfupi kabla ya Marekani na Israel kujiandaa kuanzisha shambulio dhidi ya Iran, C.I.A. ilibaini kwa usahihi eneo la lengo muhimu zaidi ambalo ni Ayatollah Ali Khamenei, kiongozi mkuu wa nchi hiyo.
C.I.A. ilikuwa ikimfuatilia Khamenei kwa miezi kadhaa, ikiongeza uhakika kuhusu maeneo yake na mienendo yake ya kawaida, kulingana na watu wanaofahamu operesheni hiyo.
Kisha shirika hilo lilipata taarifa kwamba mkutano wa maafisa wakuu wa Iran ungefanyika Jumamosi asubuhi katika makazi ya uongozi katikati ya Tehran.
Muhimu zaidi, C.I.A. iligundua kwamba kiongozi mkuu angekuwepo katika eneo hilo.
Marekani na Israel ziliamua kurekebisha muda wa shambulio lao, kwa sehemu ili kunufaika na taarifa mpya za kijasusi, kulingana na maafisa waliokuwa na ufahamu wa maamuzi hayo.
Taarifa hiyo ilifungua mlango na fursa kwa nchi hizo mbili kupata ushindi wa mapema na wa kimkakati kuwaondoa maafisa wakuu wa Iran na kumuua Ayatollah Khamenei.
Kuondolewa kwa haraka kwa kiongozi mkuu wa Iran kulionyesha uratibu wa karibu na ushirikiano wa taarifa za kijasusi kati ya Marekani na Israel kabla ya shambulio hilo, pamoja na kiwango cha juu cha uelewa waliokuwa nacho kuhusu uongozi wa Iran hasa baada ya vita vya siku 12 vya mwaka uliopita.
Operesheni hiyo pia ilionyesha kushindwa kwa viongozi wa Iran kuchukua tahadhari za kutosha ili kuepuka kujianika, wakati Israel na Marekani zilikuwa zikituma ishara wazi kwamba zilikuwa zikijiandaa kwa vita.
Kwa mujibu wa watu waliopokea taarifa hizo, C.I.A. ilipeleka Israel taarifa zake za kijasusi zilizokuwa na “usahihi wa hali ya juu” kuhusu mahali alipo Ayatollah Khamenei.
Mimi sina utaalamu wa kijasusi lakini akili yangu inanituma kwenye usaliti, njaa, vitsho, au kuchoshwa na utawala wa muda mrefu wa Ayatollah.

Post a Comment

Previous Post Next Post
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG