Nchini Comoro, serikali imerejelea hatua yake na kusitisha kupanda kwa bei ya mafuta baada ya mgomo wa siku sita uliosababisha vifo vya watu wawili na kusababisha mvutano katika visiwa hivyo. Tangazo hilo lilitolewa siku ya Jumamosi jioni mbele ya wawakilishi wa vyama vya usafiri na wafanyakazi. Tangu kuanza kwa mgomo huo siku ya Jumatatu, Mei 11, vizuizi vya barabarani, makabiliano, na kuzorota kwa shughli za kuchumi vimeikumba nchi hiyo.
Tags
VITA