BANDA MEDIA BLOG

CARLOS TEVEZ AIONGOZA BOCA JUNIOR KUTWAA KOMBE LA LIGI YA ARGENTINA

Mchezaji Carlos Tevez amepata mapokezi ya hisia kali yakichagizwa na ushindi wa jumapili wa Boca Junior baada ya kuiongoza vyema kutwaa kwa mara ya 31 kombe la Ligi ya Argentina.



Goli la kichwa kutoka kwa beki wa kushoto wa Fabian Monzon lilitosha kuipatia ushindi mwembamba Boca dhidi ya Tigre na kujihakikishia kutwaa kombe hilo kwa mara ya kwanza tangu 2011 huku wakiwa na mchezi uliobakia.



Kapteni Tevez, ambaye amerejea kuichezea timu yake ya ujana ya Boca Julai mwaka huu, baada ya kucheza ligi za nchi za nje kwa muongo mmoja, alijawa na furaha tele baaada ya kupulizwa filimbi ya wisho.

       Tevez akiwa na wachezaji wa Boca Junior wakifurahia kutwaa kombe
Carlos Tevez akishangilia mara baada ya mchezo huo 

Post a Comment

Previous Post Next Post
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG