BANDA MEDIA BLOG

KAGERA SUGAR SASA MAMBO POA, UWANJA WAO WAANZA KUWEKWA NYASI BANDIA

Uwekwaji Nyasi ukiendelea katika Uwanja wa Kaitaba leo hii.

 Taswira kamili





 Uwanja huo umeanza kuwekwa nyasi rasmi leo na ndani ya siku 14 utamalizika na taratibu nyingine zitafuata na timu ya Kagera itaanza kuutumia Uwanja huo. Uwanja huu sasa utakuwa umeongezeka katika viwanja vilivyowekwa nyasi hapa Tanzania ikiwa ni pamoja na uwanja wa uwanja wa Uhuru uliopo Dar es Salaam, uwanja wa Karume (Dar es Salaam) na uwanja wa Gombani uliopo Pemba.

 Taswira ya nyasi zenyewe za bandia zikiwa zimetandazwa katika Uwanja huo wa Kaitaba uliopo Bukoba Mjini ambao hutumiwa na timu ya  Kagera Sugar ambayo kwa sasa inaendelea kutumia uwanja vya Ali Hassan Mwinyi wa Tabora.
 Katibu wa KRFA Salumu Umande Chama ambaye pia ni kiongozi kamati ya Waamuzi nchini akizungumzia suala zima la uwanja huo wa Kaitaba na waandishi wa habari Jumatatu 02 Novemba, 2015. Chama ameeleza kutokana na kasi iliyopo na kama mafundi hawatakwama uwanja huo utamalizika ndani ya wiki mbili tu.
Na Faustine Ruta, Bukoba
Uwanja wa Kaitaba Bukoba umeanza kuwekwa nyasi bandia rasmi leo hii Jumatatu 2 Novemba, 2015 na kutokana na maelezo ya wawekaji wa nyasi hizo, wamesema utachukuwa muda wa siku 14 tu.
Wakaazi wa Mji wa Bukoba na vitongoji vyake sasa kuanza kushuhudia kipute live bila chenga katika uwanja huo wa Kaitaba.
Timu ya Kagera Sugar nayo inatarajiwa kurudi katika uwanja huo ambao huutumia kama uwanja wao wa nyumbani lakini tangu msimu uliopita wamekuwa wakitumia viwanja vingine kwa michezo yao ya nyumbani.
Uwanja wa Kaitaba  unajengwa kwa  ufadhili wa FIFA chini ya mpango wa misaada wa Goal Projects.




Post a Comment

Previous Post Next Post
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG