![]() |
| Mmoja wa wafanyakazi wa hospitali hiyo, Cresensia Joseph John akichangia mada kwenye mkutano wa Baraza la Wafanyakazi wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH). |
![]() |
Baadhi ya wafanyakazi wa Hospitali
ya Taifa ya Muhimbili (MNH) wakimsikiliza Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa
hospitali hiyo, Profesa Lawrence Mseru kwenye mkutano wa Baraza la
Wafanyakazi.
PICHA ZOTE KWA HISANI YA HOSPITALI YA TAIFA YA MUHIMBILI (MNH)
…………………………………………………………………….
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa
Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH), Profesa Lawrence Mseru leo
amekutana na Baraza la Wafanyakazi la Hospitali hii katika kikao cha 15
cha Baraza hili.
Katika kikao hicho wafanyakazi
wamezungumzia changamoto zinazoikabili MNH na mafaniko mbalimbali
yaliopatikana yakiwamo uboreshaji wa miundo mbinu na upatikanaji wa
huduma kwa kiwango cha juu.
Profesa Mseru amewataka
Wakurugenzi, Wakuu wa Idara pamoja na Mameneja wa Majengo kusimamia
vizuri wafanyakazi wa MNH watimize wajibu wao ili kuongeza tija mahali
pa kazi.
“Kila mmoja anapaswa kutekeleza
majukumu yake kwa mujibu wa sheria na mkataba wake wa kazi ili kufikia
malengo,”amesema Kaimu Mkurugenzi Mtendaji, Mseru.
Fuatilia katika picha kwa habari zaidi.
|
Tags
AFYA






