NA RAYMOND MUSHUMBUSI – MAELEZO
Timu ya wataalamu wa afya
kutoka vituo vya Afya, Bandari, Viwanja vya Ndege na mipaka ya nchi kavu
ambayo imejumuisha maafisa wa afya na mazingira, madaktari na wauguzi
kutoka Tanzania bara na Zanzibar imefanya mafunzo ya vitendo ya ukaguzi
wa meli ndani ya bandari ya Dar es salaam.
Akizungumza na waandishi wa
habari Kaimu Mratibu wa Vituo vya Afya Bandari na Viwanja vya Ndege Bw.
Remidius Kakulu amesema wataalamu hawa wapo katika mafunzo ya vitendo
yanayoratibiwa na kuendeshwa na wizara ya Afya na Ustawi wa jamii
ikishilikiana na Shirika la Afya Duniani (WHO).
Amesema malengo ya mafunzo hayo
ni kuwajengea uwezo wakaguzi wa vyombo vya usafiri zikiwemo meli na
ndege na kutoa vyeti vya usafi vya kimataifa kwa wamiliki na waendeshaji
wa vyombo hivyo. Mafunzo haya yatawezesha kuandaa vituo vyetu vya
ukaguzi kwa viwango vya kimataifa kwa mujibu wa kanuni za afya za
kimataifa za mwaka 2005.
Aidha katika ukaguzi huo
ulifanikisha kukagua meli nne(4) za mizigo na magari na kufanikiwa
kukagua sehemu kumi na tatu(13) zikiwemo sehemu za kulala
mabaharia(Quarters),sehemu za jikoni na store za kuhifadhia vyakula,
utunzajia na udhibiti wa dawa ( Medical facilities),sehemu za kuogelea(
swimming pools), udhibiti wa taka ngumu na taka zitokanazo na mabaki ya
madawa( medical wastes), upatikanaji wa maji safi na salama,udhibiti wa
maji taka,udhibiti wa umwagiliaji wa maji yanayosaidia balance ya meli (
Ballast water) na maeneo mengine ambayo yanaweza kuhatarisha afya ya
binadamu na mazingira.
Mmoja wa maafisa aliyeshiriki
mafunzo hayo Bw. Onesmo Masta Kitange Afisa Afya Mkuu Mazingira kutoka
Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere
amesema mafunzo hayo yamewasaidia kupata utaalamu zaidi na kujiamini
katika kazi zao za ukaguzi katika vyombo vya usafiri licha ya changamoto
mbalimbali.
Naye Bi Eliengera Mghase ambaye
ni Afisa Afya Mwandamizi Bandari amesema mafunzo hayo ya siku sita
(6), kwa mafunzo ya siku tano (5) ya darasani na siku moja kwa vitendo
ambayo yamewawezesha kupata utaalamu zaidi katika kazi zao za ukaguzi wa
vyombo vya usafiri vya majini na nchi kavu.
Mafunzo hayo yalijumuisha
makundi mawili tofauti likiwemo kundi la kwaqnza lilifanya mafunzo kwa
vitendo kuanzia tarehe 3/11/2015 hadi tarehe 8/11/2015 na kundi la pili
lililomalizia kutoka tarehe 10/11/2015 hadi tarehe 13/11/2015amabayo
yamewasaidi kuongeza ufanisi kutoka ukaguzi wa sehemu tatu(3) tu katika
meli mpaka kufikia sehemu kumi na tatu (13) hivyo kuongeza weledi
kwenye kazi zao hasa kudhibiti mapungufu yanayojiyokeza.
Tags
AFYA
