BANDA MEDIA BLOG

UNATAKA KUWAZUIA WARRIORS? BASI KAA TAYARI WANAKUJA KUKUTEMBELEA. WAWEKA REKODI YA USHINDI DHIDI YA TIMBERWOLVES

Stephen Curry alifunga pointi 46, huku 21 zikiwa katika robo ya kwanza, na kuisadia Golden State Warriors kuboresha rekodi yake ya ushindi kuwa 10-0 katika ushindi wa 129-116 dhidi  ya Minnesota Timberwolves Alhamisi usiku.

Draymond Green alikuwa na pointi 23, pasi 12 na rebounds8  kwa Warriors, ambao wanakuwa ni mabingwa watetezi wa nne kuanza msimu na angalau ushindi mara 10 mfululizo pasi na kupoteza. Curry alipata mitupo  15 kati ya  25aliyojaribu, ikiwa ni pamoja na mitupo  8 kati ya 13  kutoka katika eneo la point 3.
Karl- Anthony Towns alimaliza  na pointi 17 na 11 rebounds na Andrew Wiggins alifunga pointi 19 kwa Minnesota Timberwolves ( 4-4 ) , ambao wamepoteza michezo yote minne ya  nyumbani msimu huu.
Celtics katika misimu ya 1957-1958 na 1964-1965 na Chicago Bulls katika msimu wa 1996-1997 zinakuwa timu nyingine pekee ambazo zilikuwa mabingwa watetezi katika NBA na kuweza kuanza msimu kwa ushindi mara 10 mfululizo.
Mwaka jana Russell Westbrook aliongoza  NBA kwa kufunga point 20 katika robo moja mara nne tofauti. Mpaka sasa Stephen Curry tayari ana robo nne ambazo ameweza kufunga point 20 au zaidi na ni  katika michezo 10 pekee.

Post a Comment

Previous Post Next Post
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG