BANDA MEDIA BLOG

Zaidi ya wagonjwa 200 kutoka maeneo mbalimbali mkoa wa Arusha wapewa elimu kutambua vyanzo vya magonjwa


Na Gladness Mushi,Arusha
ZAIDI ya wagonjwa 200 kutoka maeneo mbalimbali katika mkoa wa Arusha wamefanikiwa kupewa elimu ya kutambua vyanzo vya magonjwa yao pamoja na kuepukana na mbinu mbalimbali ambazo zinafanywa na wataaalamu wa afya kwa malengo ya kupata faida
Hataivyo Elimu hiyo imetolewa na Hospitali ya Shree Hindu Union Charitable iliopo maeneo ya Faya jijini Arusha ambapo elimu hiyo inatolewa bure kwa kila siku.

Akiongea na waandishi wa habari kuhusiana na mpango huo wa utoaji wa elimu, mganga mkuu wa hospitali hiyo Dkt Rajendra Patama alisema kuwa lengo halisi la kuanzisha mpango huo ni kuweza kuwaokoa watanzania ambao mara nyingi wanadanganyika kuwa wanaumwa na kumbe hawaumwi.
Rajendra alifafanua kuwa mpango huo umeanza hivi karibuni kwani kwa sasa wapo baadhi ya wataalamu wa afya ambao wanatumia mwanya wa wagonjwa kuumwa na kisha kuwabambikiza magonjwa ambayo sio yao ili waweze kuapata viapato vyao vya kila siku
Dkt huyo alidai kuwa hali hiyo inawafanya wagonjwa wengi kuishi kwa wasiwasi huku kwa upande wa wengine nao wakijikuta wanatumia dawa ingawaje hawaumwi na chochote hali ambayo nayo inasababisha miili kujaa sumu kubwa sana.
“Hapa kila siku lazima tutoe elimu ya magonjwa mbalimbali lakini hata kiiini cha magonjwa yanayoambukiza na yale ambayo hayaambukizi na ambao wameshapata elimu hii kwa kweli hawawezi kutapeliwa bali wanachukua tahadhari tuu wao na jamii zao”aliongeza.
Wakati huo huo alisema kuwa kwa kutambua umuhimu wa tiba kwa watanzania wameshaweza kuwasafirisha wagonjwa 6 nje ya nchi kwa ajili ya kuweza kufanyiwa vipimo na tiba kubwa na mpaka sasa hali za wagonjwa hao zinaenedelea vema.
“Huu mkakati wetu wa kuepukana na vifo visivyo vya lazima pamoja na kutoa elimu umeweza kuwasafirisha wagojwa 6 na bado tupo kwenye mchakato wa kuwasidia walio wengi zaidi”alisisitiza Dkt huyo.
Alimalizia kwa kuwataka watanzania hususani wanawake kuhakikisha kuwa wanajiwekea utaratibu wa kupima afya zao kila mara na pia kujitokeza kwa wingi kwani wanatarajia kutoa wataalamu wa masuala mbalimbali ya afya kutoka Nchini India.

Post a Comment

Previous Post Next Post
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG