Na Gladness Mushi,Arusha
Hataivyo Elimu hiyo imetolewa na
Hospitali ya Shree Hindu Union Charitable iliopo maeneo ya Faya jijini
Arusha ambapo elimu hiyo inatolewa bure kwa kila siku.
ZAIDI ya wagonjwa 200 kutoka
maeneo mbalimbali katika mkoa wa Arusha wamefanikiwa kupewa elimu ya
kutambua vyanzo vya magonjwa yao pamoja na kuepukana na mbinu mbalimbali
ambazo zinafanywa na wataaalamu wa afya kwa malengo ya kupata faida
Hataivyo Elimu hiyo imetolewa na
Hospitali ya Shree Hindu Union Charitable iliopo maeneo ya Faya jijini
Arusha ambapo elimu hiyo inatolewa bure kwa kila siku.
Akiongea na waandishi wa habari
kuhusiana na mpango huo wa utoaji wa elimu, mganga mkuu wa hospitali
hiyo Dkt Rajendra Patama alisema kuwa lengo halisi la kuanzisha mpango
huo ni kuweza kuwaokoa watanzania ambao mara nyingi wanadanganyika kuwa
wanaumwa na kumbe hawaumwi.
Rajendra alifafanua kuwa mpango
huo umeanza hivi karibuni kwani kwa sasa wapo baadhi ya wataalamu wa
afya ambao wanatumia mwanya wa wagonjwa kuumwa na kisha kuwabambikiza
magonjwa ambayo sio yao ili waweze kuapata viapato vyao vya kila siku
Dkt huyo alidai kuwa hali hiyo
inawafanya wagonjwa wengi kuishi kwa wasiwasi huku kwa upande wa wengine
nao wakijikuta wanatumia dawa ingawaje hawaumwi na chochote hali ambayo
nayo inasababisha miili kujaa sumu kubwa sana.
“Hapa kila siku lazima tutoe elimu
ya magonjwa mbalimbali lakini hata kiiini cha magonjwa yanayoambukiza
na yale ambayo hayaambukizi na ambao wameshapata elimu hii kwa kweli
hawawezi kutapeliwa bali wanachukua tahadhari tuu wao na jamii
zao”aliongeza.
Wakati huo huo alisema kuwa kwa
kutambua umuhimu wa tiba kwa watanzania wameshaweza kuwasafirisha
wagonjwa 6 nje ya nchi kwa ajili ya kuweza kufanyiwa vipimo na tiba
kubwa na mpaka sasa hali za wagonjwa hao zinaenedelea vema.
“Huu mkakati wetu wa kuepukana na
vifo visivyo vya lazima pamoja na kutoa elimu umeweza kuwasafirisha
wagojwa 6 na bado tupo kwenye mchakato wa kuwasidia walio wengi
zaidi”alisisitiza Dkt huyo.
Alimalizia kwa kuwataka watanzania
hususani wanawake kuhakikisha kuwa wanajiwekea utaratibu wa kupima afya
zao kila mara na pia kujitokeza kwa wingi kwani wanatarajia kutoa
wataalamu wa masuala mbalimbali ya afya kutoka Nchini India.
Tags
AFYA