Farid Musa (kulia) akichuana na Wiliam Otong wa Africa Lyon
Timu za ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara bado zimeendelea kutoa dozi
kwenye michuano ya Azam Sports Federation Cup baada ya leo Azam FC
kutoa kichapo cha magoli 4-0 kwa Africa Lyon FC mchezo uliopigwa kwenye
uwanja wa Karume, Dar es Salaam. Golikipa wa African Lyon Hamad Juma akiondosha mpira kwenye eneo la hatari mbele ya Ame Ally
Magoli ya Azam FC yamefungwa na Mudathir Yahya aliyefunga bao la
kwanza dakika ya kwanza ya mchezo kisha Farid Musa akapachika bao mbili
wavuni dakika ya 8 na 37 kipindi cha kwanza na kuufanya mchezo huo
kwenda mapumziko huku Azam wakiwa mbele kwa bao 3-0 dhidi ya Africa
Lyon. Nahodha na mshambuliaji wa Azam FC John Boco ‘Adebayor’ akitia krosi langoni mwa Africa Lyon
Kipindi cha pili Azam waliendeleza kisago kwa Africa Lyon baada ya
Ame Ally kuifungia timu yake bao la nne na kukamilisha ushindi wa Azam
kwenye mchezo huo. Shomari Kapombe wa Azam FC (katikati) akiwa amekusanya ‘kijiji’ cha Africa Lyon akitmea nacho
Azam inaungana na timu nyingine kusonga mbele kwa hatua ya 16 bora
kwenye michuano ya FA ambayo bingwa wake ataiwakilisha Tanzania kwenye
michuano ya kombe la Shirikisho barani Afrika msimu ujao. Wiliam Otong wa Africa Lyon (kushoto) akimkabili Farid Musa wa Azam FC