Wanachama wa klabu ya Yanga wameibuka makao makuu ya klabu yao kupinga kujiuzulu kwa aliyekuwa katibu mkuu wa klabu hiyo Dr. Jonas Tiboroha ambaye inaelezwa amechukua uamuzi huo kutokana na shinikizo kutoka kwa mwenyekiti wa klabu hiyo Yusuf Manji.
Leo imetoka taarifa kwamba Dr. Tiboroha ametangaza rasmi kujuzulu wadhifa wake na ameshakabidhi barua ya kuachia nafasi hiyo huku akisema kwa sasa anataka aendelee na maisha yake ya kazi nyingine lakini si ya kuiongoza klabu ya ‘Wana Jangwanni’.
Mara baada ya taarifa hizo kuwafikia wanachama, mashabiki na wapenzi wa Yanga, walikusanyika kwenye makao makuu ya ofisi za klabu yao wakipinga kujiuzulu kwa Dr. Tiboroha uku wakidai hilo ni shinikizo na si maamuzi kamili ya katibu huyo.
Picha za matukio mbalimbali kama yalivyonaswa na camera yetu ya shaffihdauda.co.tz ‘Timu ya Ushindi’.
Tags
MICHEZO KITAIFA