Waogeleaji wakionyesha staili ya kuogelea ‘kinyume nyume’ katika moja ya mazoezi ya klabu ya Dar Swim Club.
Peter Itatiro wa Dar Swim Club akionyesha umahiri wake
katika kuogelea. Peter ana miaka 9 atashiriki katika aina nne ya
mashindano hayo kwa staili zote.
Waogeleaji wa klabu ya Dar Swim
Club walifanya mazoezi kwa ajili ya mashindano ya Tallis yaliyopangwa
kuanza Ijumaa kwenye bwawa la kuogelea la Shule ya Kimataifa ya
Tanganyika (IST) Upanga.
……………………………………………………………………………………
Na Mwandishi wetu
Timu ya kuogelea ya Isamilo kutoka mkoa wa Mwanza na Dar Swim Club zimetamba kutwaa nafasi ya kwanza katika
mashindano ya kuogelea ya Tallis yaliyopangwa kuanza Ijumaa
Januari 29 na kumalizika Jumamosi Januari 30 kwenye bwawa la kuogelea la
Shule ya Kimataifa ya Tanganyika ( IST Upanga).
Akizungumza kwa njia ya simu
kutoka Mwanza jana, Mwenyekiti wa Klabu ya Kuogelea ya Mwanza (MSC),
Jason Miller alisema kuwa wamejiandaa vilivyo kutwaa medali za dhahabu
katika mashindano hayo amayo yatafanyika kwa siku mbili.
Miller alisema kuwa klabu ya
Isamilo ndiyo inawakilisha mkoa huo katika mashindano hayo ambayo
yanatarajiwa kushirikisha waogeleaji zaidi ya 400 kutoka klabu
mbalimbali hapa nchini.
Alisema kuwa wamecagua
waogeleaji 21 kwa ajili ya mashindano hayo na kwa muda wote walikuwa
katika mazoezi makali. “Najua kuna ushindani mkubwa sana katika
mashindano , tulifanya mazoezi kwa muda mrefu na kuwashindanisha staili
mbalimbali za kuogelea kwa kuzingatia muda, wote wameonyesha muda mzuri
na tupo tayari kwa mashindano,” alisema Miller.
Aliwataja wachezaji wake kwa
upande wa wasichana kuwa ni Anna Guild, Emma Imhoff, Bridget Peck,
Rebecca Guild, Nandi O’Sullivan, Natalie Mulford, Sachi Buggana,
Sofia Sanchez, Isobel Sanchez, Umi Kulthum na Maisah Pirani.
Kwa upande wa wavulana ni
Matthew Guild, Elia Imhoff, Eric Nixon, Khaleed Razac, Judah Miller,
Caleb O’Sullivan, Delvin Barick, Jack Peck, Daniele Imhoff na Ezra
Miller.
Wakati Isamilo ikitamba, klabu
maarufu ya Dar Swim Club nayo imetamba kulibakisha taji la mashindano
hayo kutokana na mazoezi ambayo wameyafanya.
Katibu Mkuu wa Dar Swim Club,
Inviolata Itatiro alisema jana kuwa wamejiandaa vilivyo kwa ajili ya
kutwaa medali nyingi za zawadi na hasa ukizingatia kuwa waogeleaji wao
wana uzoefu wa kimataifa.
Inviolata alisema kuwa hivi
karibuni walifanya vyema katika mashindano yaliyofanyika nchini Dubai na
kushirikisha waogeleaji kutoka nchi mbalimbali duniani huku wao wakiwa
wanashiriki kwa mara ya kwanza.
“Tulishinda medali za dhahabu
katika mashindano hayo, waogeleaji wetu wamepata uzoefu mkubwa, naamini
watafanya vyema,” alisema Inviolata ambapo jumla ya waogeleaji 50
wataiwakilisha klab hiyo.
Waogeleaji hao ni Meyia Avery,
Anna Azzoni, Chinwe Bruns, Joshua Bruns, Isobel Bush, Klaryce Durand,
Smriti Gokan, Bailey Golembeski, Carter Golembeski, Celina Itatiro,
Lidia Janik, Ursulla Khimji, Mayli Kiepe, Naaliyah
Kweka, Saffiro Kweka, Lois
Scheren, Diya Shah, Maya Somaiya, Niki Somaiya, Kelya Temba, Maia
Tumiotto, Lara Van Den Hombergh na Chichi Zengeni ambao ni wasichana.
Kwa upande wa wavulana ni
Timothee Callens, Sebastian Carpintero, Raahi Davda, Jean De Villard,
Marin De Villard, Victoire De Villard, Flore De Villeneuve, Gaspard De
Villeneuve, Luwe De Wet, Joaquim Deering, Lisa Di Stefano,Josh
Golembeski,Matt Golembeski, Peter Itatiro, Jonathan, Lubuva, Adrien
Madjitoloum, Reuben Monyo, Emmanuele Moroni, Rodolfo Moroni, Thierry
Murunga, Christopher Nikitas, Ishaan Patel, Victor Richmond, Kees
Rodenburg, Neel Ruparelia, Arjun Taylor na Alessandro Tumiottoends…
Mratibu wa mashindano hayo,
Alexander Mwaipasi alisema kuwa maandalizi yanaendelea vizuri na timu
zaidi ya 15 zitashiriki katika mashindano hayo. “Timu nyingi zimetuma
majina ya waogeaji wao na zipo tayari kwa mashindano,” alisema Mwaipasi.
Tags
MICHEZO KITAIFA