BANDA MEDIA BLOG

KICHUYA AMLILIA MWAMUZI ALIYEFUNGIWA KUCHEZESHA MAPINDUZI CUP KWA KUKATAA GOLI LAKE

Winga wa Mtibwa Sugar Mohamed Kichuya ambaye alifunga goli lililokataliwa wakati wa mechi kati ya Mtibwa vs Azam
Winga wa Mtibwa Sugar Mohamed Kichuya alifunga goli lililokataliwa wakati wa mechi kati ya Mtibwa vs Azam, mwamuzi Danila Mtwana ambaye ameondolewa kwnye orodha ya waamuzi wa Mapinduzi Cup
Mohamed Kichuya ambaye ndiyo mfungaji wa goli ambalo lilikataliwa na mwamuzi Dalila Jaffar Mtwana amesema amesikitishwa na uamuzi uliotolewa na kamati ya ZFA ya kumuondoa mwamuzi huyo kwenye orodha ya waamuzi watakaoendelea kuchezesha mashindano ya Mapinduzi Cup.
Kichuya ameiambia shaffihdauda.co.tz kuwa, yeye binafsi amesikitishwa na taarifa hiyo kwasababu yeye (mwamuzi) pia ni binadamu na anaweza kukosea kama binadamu wengine lakini akaongeza kuwa u-referee ni kazi yake ambayo inampatia kipato na kumfungia ni kumzua asipate pesa ambayo alikuwa anapata kutoka kwenye mashindano hayo.
“Unajua yule pia ni binadamu, huenda ilikuwa ni kosa la kibinadamu kwahiyo siwezi kumlaumu sana kwasababu labda hata angekuwa mwamuzi mwingine angekosea pia”, amesema Kichuya ambaye goli lake lililokataliwa ndiyo limemwondoa mwamuzi huyo kwenye mashindano.
“Lakini kibaya na kinachonisikitisha ni kwamba, ureferee ni kazi yake inayomuingizia kipato hivyo kumfungia inaamaana kwamba hapati tena miambili-miambili alizokuwa anazipata kutokana na mashindano haya”.
Lakini Kichuya amewaonya waamuzi kuwa makini muda wote wa mchezo ili kuzuia makosa ambayo yanaweza kuepukika ili kukwepa lawama pamoja na kufungiwa ili kuufanya mchezo wa soka kuwa mchezo wa kiungana.

Post a Comment

Previous Post Next Post
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG