SAMATTA ATIMKIA NIGERIA KUTAFUTA HESHIMA YA TANZANIA
byJohn Banda-
0
Mbwana
Samatta (katikati) akiwa sambamba na Katibu Mkuu wa TFF Mwesigwa
Selestine (kulia) pamoja na mwandishi na mchambuzi wa michezo wa Clouds
Media Group na shaffihdauda.co.tz
Mambo tayari yameshaiva, mshambuliaji nyota wa Tanzania Mbwana
Samatta ameiacha ardhi ya Bongo usiku wa kuamkia leo (January 6, 2015)
na kupaa kuelekea jijini Abuja, Nigeria kwenye sherehe za ugawaji wa
tuzo za mchezaji bora Afrika kwa mwaka 2025 (Glo-CAF Awards) ambazo
zitakabidhiwa kwa washindi January 7, 2026.
Samatta ameingia fainali ya kinyang’anyiro cha tuzo ya mchezaji bora
Afrika 2015 anayecheza soka ndani ya Afrika baada ya kupata mafanikio
makubwa na klabu yake ya TP Mazembe kwa mwaka 2015. Mbwana
Samatta akifanyiwa mahojiano na kituo cha television cha Azam TV muda
mfupi kabla ya kuondoka kwenye uwanja wa ndege jijini Dar es Salaam
kuelekea Abuja
Samatta ameisaidia Mazembe kutwaa ubingwa wa klabu bingwa barani
Afrika lakini pia akiibuka mfungaji bora wa mashindano kwa kufikisha
jumla ya magoli saba (7) sawa na mshambuliaji Bakri Almadina anayekipiga
kwenye klabu ya Al-Marreikh Omdurman ya Sudan.
Samatta ameingia fainali kuwania uzo hiyo pamoja na mchezaji mwenzake
wa timu moja Robert Kidiaba ambao wote kwa pamoja waliiwezesha TP
Mazembe kunyakua ubingwa wa Afrika kwa ngazi ya vilabu lakini pia kwenye
orodha hiyo ya wachezaji watatu yupo mshambuliaji wa kimataifa wa
Algeria Baghdad Bounedjah anayecheza klabu ya Etoile du Sahel ya Tunisia
ambaye pia ameisadia klabu yake kutwaa ubingwa wa kombe la shirikisho
barani Afrika. Mwandishi
na mchambuzi wa michezo Shaffih Dauda akihojiwa na kituo cha Azam TV
muda mfupi kabla ya kuondoka uwanja wa ndege jijini Dar es Salaam
kuelekea Abuja-Nigeria kushuhudia ugawaji wa tuzo za wanamichezo
waliofanya vizuri mwaka 2015
Endapo Samatta atafanikiwa kutwaa tuzo hiyo ataingia kwenye kitabu
cha rekodi ya kuwa mtanzania wa kwanza kutwaa tuzo ya mcheaji bora wa
Afrika ukiachana na rekodi waliyoweka yeye na Ulimwengu ya kuwa
watanzania wa kwanza kutwaa ndoo ya klabu bingwa Afrika.
Siku chache kabla ya Samatta kuelekea nchini Nigeria, alimtembelea
Waziri mwenye dhamana ya michezo Mh. Nape Nnauye ambaye kwa niaba ya
serikali, Nnauye alimpa Samatta Baraka zote kuelekea tuzo hizo huku
akimtabilia Samatta kuibuka mshindi kwenye kinyang’anyiro hicho.