BANDA MEDIA BLOG

MAJALIWA: TANZANIA ITAENDELEA KUSHIRIKIANA NA RWANDA

rw1
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Balozi wa Rwanda nchini, Mhe. Eugene Kayihura kabla ya mazungumzo yao, Ofisini kwa Waziri Mkuu jijini Dar es salaam Januari 13, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

rw2
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika ya Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Dkt. Augustine Mahiga (kulia) akizungumza na Balozi wa Rwanda nchini, Mhe. Eugene Kayihura walipokutana Ofisini kwa Waziri Mkuu jijini Dar es salaam Januari 13, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
rw3
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Balozi wa Rwanda nchini, Mhe. Eugene Kayihura  Ofisini kwake  jijini Dar es salaam Januari 13, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)


WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa amekutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Rwanda nchini, Eugene Kayihura. Ambapo amemuahidi kuwa Tanzania itaendelea kushirikiana na Rwanda.
Akizungumza na Balozi  Kayihura  jana ,(jumatano 13, 2016) ofisini kwake, Magogoni jijini Dar es salaam, Waziri Mkuu amemshukuru  Balozi huyo kwa kumtembelea na ameahidi kuwa Serikali ya Tanzania itaendeleza ushirikiano ulipo baina ya nchi hizi mbili.
 “Nia yetu ni kushirikiana kwa pamoja kwa kuunganisha wafanyabiashara wetu, kwa kutumia Bandari  ya Dar es salaam na reli ya kati, ambayo tutajenga kwa  kiwango cha kisasa ‘standard gauge’  ili ziweze kubeba mizigo mingi na kwenda mwendo wa kasi” alisema Waziri Mkuu.
Kwa upande wake, Balozi wa Rwanda, Kayihura amesema Tanzania na Rwanda ni nchi marafiki na zinafanyakazi wa pamoja, Rwanda iko tayari kushirikiana na Tanzania kikanda na kimataifa.
“Tunatumia Bandari ya Dar es salaam na Mombasa, tunashukuru kwa namna ambavyo mnaboresha Bandari ya Dar es Salaam, kwani Rwanda inafaidika pia kwa vile mizigo yetu mingi karibu asilimia 75 husafirishwa  kupitia bandari hii”  alisema Balozi Kayihura

Post a Comment

Previous Post Next Post
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG