Mkurugenzi Mkuu wa
Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Mhandisi Suleiman Said
amefariki dunia mapema leo asubuhi akiwa katika mazoezi ya
kuogelea,taarifa zinaeleza kuwa baada ya tukio hilo Bwa.Suleiman
alikimbizwa hospitali ya Agakhan kwa matibabu,na baadae ikaelezwa kuwa
amekwishafariki na kuwa mazishi yanatarajiwa kufanyika leo. Marehemu
alipata kuwa Katibu mkuu wa Simba.
Taarifa zaidi zinasema Marehemu
Mr Sukeiman aliamka asubuhi akamwambia mke wake hajiskii vizuri, lakini
alienda baharini kuogelea kama kawaida yake. Walikuwa wawili na mwenzie,
wakaenda mbali sana wakati wa kirudi aliishiwa nguvu, alijitahidi
akafika nchi kavu akiwa hoi kabisa amekunywa maji wengi na akawa
anatokwa na mapovu mdomoni. Alifariki njiani akipelekwa hospitali. Msiba
upo upanga nyuma ya jeshi (Ngome) saa hii maiti imefuatwa wanakuja
kuaga hapa nyumbani, mwili utarudi msikitini saa tisa kisha kuzika
makaburi ya Kisutu nyuma ya chuo cha CBE. Apumzike kwa Amani.
Tags
HABARI KITAIFA