BANDA MEDIA BLOG

JESHI LA POLISI MKOA WA KIPOLISI KINONDONI LAKAMATA WEZI NA WAHARIBIFU WA MIUONDOMBINU YA TANESCO

 Mkuu wa kitengo cha mawasiliano Tanesco  Leila Muhaji akizungumza na waandishi wa kuhusu wizi  wa vifaa vya umeme vyenye thamani ya milioni 61 vilivyokamatwa jijini Dar es salaam,Kulia ni Kaimu Kamishna wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam,Lucas Mkondya.
  Kaimu Kamishna wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam,Lucas Mkondya.(wa pili kushoto) akiwa na waandishi na walinzi wa Tanesco.
  Kaimu Kamishna wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam,Lucas Mkondya.(wa pili kushoto) akiwa na waandishi.

  Kaimu Kamishna wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam,Lucas Mkondya.(wa pili kushoto) akiwa na waandishi.
 Gari la Tanesco likiwa na shehena ya vifaa vilivyokamatwa katika kituo   Kikuu cha Polisi Dar es Salaam.
Gari la Tanesco likiwa na shehena ya vifaa vilivyoibwa katika kituo   Kikuu cha Polisi Dar es Salaam. 
Mwandishi Wetu.
 Jeshi la Polisi Mkoa wa Kipolisi Kinondoni likishirikiana na Kikosi kazi cha kuzuia uharibifu wa miondo mbinu ya Shirika la umeme Tanzania Tanesco Tarehe 18-10.2016 saa 10;00 jioni lilipata taarifa toka kwa raia mwema kuwa katika  maeneo ya Salasala huko Kinondoni jijini Dar es salaam kuna watu wanaoiba na  kuhuhujumu miundo mbinu ya Shirika hilo.
Kikosi hicho kilifika eneo hilo katika nyumba ya Willfred Barutti (45) mkazi wa Makumbusho na kufanya upekuzi kwenye nyumba hiyo ambapo walivipata vifaa mbalimbali Line Meterial ambavyo hutumika kwa ajili ya kuunganisha umeme  mali ya shirika la   Tanesco.
Polisi walikwenda katika nyumba nyingine mali ya Betrice Emmanuel (42) mkazi wa Salasala Mabanda wakafanya upekuzi na kufanikiwa kukamata vifaa vifuatavyo;
Nyaya aina ya Drums’02,roller ya waya aina ya AICC ya umeme wa 50 mm ambazo hutumiwa na Tanesco kituo cha Kilimahewa huko Kawe Wilaya ya Kinondoni.
Thamani ya vifaa hivyo vinakadiliwa kuwa Tsh.61,000,000,Watuhumiwa wawili wanashikiliwa kwa mahojiano na Upelelezi utakapokamilika watapelekwa mahakamani kwa hatua za kisheria.

Post a Comment

Previous Post Next Post
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG