Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais
Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa [TAMISEMI] George SimbaChawene amewagiza Wakuu wa Mikoa nchini kuhakikisha maadhimisho ya siku ya walemavu yanayoanzimishwa Duniani kote yanafanyika katika mikoa yao badala ya kukusanyika jijini Dar-es-salaam
Akiongea kwa niaba ya Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, Waziri Simbachawene amesema tamko hilo lilitokana na ombi la Chama Cha Walemavu kuomba halmshauri za wilaya ziwasafirishe wanachama wa vyama vya walemavu ili wafanye maadhimisho hayo kitaifa jijini Dar-es-salaam Desemba3,2016
‘’kwa hiyo nichukue nafasi
hii kuwaagiza wakuu wa mikoa na halmashauri
kuhakikisha wanatoa ushirikiano
wa kutosha kwa vyama vya walemavu ili viweze kufanikisha maadhimisho
hayo” Alisisitiza Simbachawene.
Simbachawene ametoa
agizo kwa mkoa wa Dar-es-salaam kufanikisha sherehe hizo katika halmashauri
zake zote, “Mkuu wa Mkoa Paul Makonda anapaswa kuchukua hatua kwa kushirikiana na halmashauri zote za
Dar-es-salaam, ahakikishe maadhimisho hayo yanafanikiwa kwa kuwapa msaada wote
unaostahili”
Vilevile amesema, “kwa kufanya hivyo hii itasaidia kupunguza gharama badala ya walemavu
wa vyama hivyo wote wangetoka kwenye wilaya zetu kuja Dar-es-salaam, sasa
shughuli hizo zifanyike maeneo ya mikoa
yao na wilaya zao na natoa maelekezo
hayo kwa sababu muda wa kufanya maadhimisho hayo ni mchache na
kuanzia leo nimeamua kutumia njia hii ili tuweze kuwasiliana kwa haraka.” alisema
Aidha Simbachawene ametoa
pongezi kwa vyama vyote vya walemavu
nchini kwa namna wanavyoshirikiana na kutoa maoni yao kwa Serikali, lakini pia Serikali ipo pamoja nao
na wataendelea kushirikiana nao kuweka mbele maslahi yao, kutatua matatizo yao na katika hili shughuli
ya kuadhimisha siku ya walemavu duniani Serikali ipo pamoja nao .
Tags
HABARI KITAIFA