BANDA MEDIA BLOG

SIMABACHAWENE AWATAKA WATUMISHI TAMISEMI KUFUATA KANUNI ZA UTUMISHI WA UMMA


Waziri wa Nchi Mhe. George B.Simbachawene (MB) akitoa hotuba kwa Baraza la Wafanyakazi lililofanyika katika Ukumbi wa Hazina ndogo mjini Dodoma ambapo amewataka kuongeza tija mahali pa kazi, kuwa na utendaji unaojali matokeo na kuepuka utendaji wa mazoea, Nidhamu na utendaji wa Watumishi wa Umma, kufanya mapitio yanayozingatia ubora katika utekelezaji wa majukumu kwa Ofisi ya Rais TAMISEMI kama taasisi na maadili kama nguzo muhimu ya kuepuka vitendo vya ubadhilifu na rushwa mahali pa kazi.

Katibu Mkuu Ofisi ya Rais TAMISEMI Mhandisi Mussa Iyombe akifafanua jambo kuhusu utekelezaji wa maagizo ya Viongozi wa juu na kuwatumikia wananchi kwa kupunguza changamoto zilizo katika Mamlaka za Serikali za Mitaa, mara baada ya Waziri wa Nchi kushoto kwake Mhe. George B.Simbachawene (MB) kutoa hotuba yake kwa Baraza la Wafanyakazi lililofanyika katika Ukumbi wa Hazina ndogo mjini Dodoma

Waziri wa Nchi  Mhe. George B.Simbachawene (MB) katika  picha ya pamoja na Wajumbe wanaounda Baraza la Wafanyakazi la Ofisi ya Rais TAMISEMI na taasisi zake DART, LAPF, Chuo cha Serikali za Mitaa Hombolo (LGTI) na Bodi ya Mikopo ya Serikali za Mitaa waliokaa kulia kwake Katibu Mkuu Ofisi ya Rais TAMISEMI Mhandisi Mussa Iyombe , Mohamed Pawaga Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu (DAHRM TAMISEMI), Susan Chekani Mkurugenzi wa Tawala za Mikoa TAMISEMI na kushoto kwake ni Katibu wa Tawi la TUGHE TAMISEMI BW. Kepha Kupa, Mchenya M.John Katibu wa TUGHE mkoa wa Dodoma na Bw. Akida mjumbe wa TUGHE kutoka Ofisi ya Rais TAMISEMI




Na Fred Kibano

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. George Simbachawene  amewataka watumishi  kufanya kazi kwa  kufuata kanuni na taratibu  za utumishi  na kuongeza tija mahali pa kazi na kujitathmini iwapo wamekidhi matarajio ya Watanzania kwa kupata huduma bora.
Mhe. Simbachawene ameyasema hayo wakati akitoa hotuba ya ufunguzi wa kikao cha Baraza la Wafanyakazi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa  (TAMISEMI) kilichofanyika  katika ukumbi wa hazina ndogo mjini Dodoma.
 ‘’kila mmoja anapaswa kutafakari haki zake na zile anazopewa je zina usawa, kwani watumishi wengi wanadhani ni marupurupu ama kuongezewa mshahara  kwani ni zaidi ya  hayo ikiwemo namna anavyochukuliwa na namna anavyo adhibiwa pale anapokosea  na kupewa pongezi pale wanapofanya vizuri’’ Alisema Mhe. Simbachawene
Pia Mhe. Simbachawene amesema Wakuu wa kila Idara na Vitengo na watumishi wanapaswa kutatua tatizo la ubinafsi kwani mfanyakazi anapofanya vizuri ni yeye ndiye anayepaswa kupewa pongezi na siyo bosi wake kujiongezea mshahara, ‘’Sisi Viongozi tunapaswa kutafakari mwisho wa siku tunafanya vizuri ama tunaumizana’’, Alisisitiza Mhe. Simbachawene.
Vilevile, Mhe. Simbachawene amesema kuna umuhimu wa kujua kila shilingi inayotumikaje na lazima ionyeshe matokeo yake ni nini na kila robo mwaka ya Utekelezaji wa Bajeti kwani kwa kufanya hivyo itawasaidia sana na kuongeza ufanisi wa kazi,  ‘’ifike wakati tunafanya yanayopaswa kufanywa,sisi ni watumishi wazuri ila tatizo linakuja kwenye utekelezaji kwani dhana ya uwajibikaji wa Umma, nidhamu ya Utumishi wa Umma inapaswa  iendelee kuimarika’’
Ameonya kuwepo kwa hali ya rushwa hasa kutoka kwa walimu wanaohitaji kuhamia sehemu nyingine kwani kuna watu wameanzisha vijiwe  mitaani na kutumia tovuti zisizo rasmi kwa kutapeli fedha  za walimu wanaohitaji huduma hiyo, hivyo basi   Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa inaendelea  na uchunguzi na  kwa wale watakaobainika hatua kali zitachukuliwa dhidi yao.

Mhe. Simbachawene alihitimisha kwa kusema ‘’kauli ya hapa kazi tu inapaswa kutekelezwa na watumishi ili kufuata taratibu na kanuni za kikazi na jukumu la kusimamia Serikali za mitaa na Halmashauri ni letu sote  kwani suala la maadili ni muhimu ili kuepuka vitendo vya rushwa.”







Post a Comment

Previous Post Next Post
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG