*Asema atafuatilia ajue kwa nini kuna tozo kwenye maghala
ya Serikali
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema
Serikali haitavumilia kuona mamia ya vijana waliofaulu mitihani ya darasa la
saba na kuchaguliwa kuingia kidato cha kwanza wanabaki nyumbani eti kwa kuwa
hakuna madarasa ya kutosha.
“Serikali haitaridhika kuona vijana
waliofaulu vizuri wanashindwa kwenda kidato cha kwanza. Halmashauri zilijua
tangu mapema ni wanafunzi wanaenda shule za msingi kwa hiyo inataka kuona wote
waliofaulu wanakwenda sekondari kwa asilimia 100,” amesema.
Ametoa kauli hiyo leo mchana wakati
akizungumza na viongozi na watendaji wa mkoa wa Lndi mara baada ya kupokea
taarifa ya mkoa huo kwenye Ikulu ndogo wilayani Nachingwea. Waziri Mkuu
amewasili wilayani Nachingwea akiwa njiani kuelekea Ruangwa kwa mapunziko ya
mwisho wa mwaka.
Amesema Serikali ya awamu ya tano
imedhamiria kutoa elimu ya bure kwa kila mtoto sasa iweje watoto wengine
wanafaulu na wanashindwa kujiunga na elimu ya sekondari. “Tumesema elimu ni
bure hakuna sababu ya kufanya wengine wasiende shule wakati azma ya Serikali ni
kutoa elimu ya bure. Hakikisheni wote wanaingia katika chaguo la kwanza,” amesema.
Amewataka Wakuu wa Wilaya na
Wakurugenzi wa Halmashauri ambazo zimefaulisha wanafunzi lakini hazina madarasa
na madawati ya kutosha warudi mezani na kujipanga upya ili kuhakikisha
wanafunzi wote waliofaulu wanapangwa na kuanza na wenzao katika chaguo la
kwanza kwani wakisubiri chaguo la pili wanakuwa wamechelewa.
“Kama tumepokea vijana wengi kwenye
udahili wa kidato cha kwanza, ni dhahiri kuwa ,tutapata Vijana wengi
watakaomaliza kidato cha nne. Sote tunajua kuna agizo la kila tarafa kuwa na
sekondari moja ya kidato cha tano na sita, nataka utekelezaji wa agizo hili
usimamiwe kuanzia sasa.”
“Tafuteni moja kati ya shule kwenye
tarafa zenu na ipandishwe hadhi kwa kuwekewa miundombinu inayotakiwa ya bwalo,
jiko, mabweni, mifumo ya maji, madarasa na vyoo vya kutosha,” amesema.
Tags
ELIMU