Mabondia Mesharck Mwankemwa wa
Mbeya na Mbwana Matumla wakioneshana ubabe makonde wakati wa mazoezi
kabla ya mpambano wao Feb. 5 / 2017 utakayofanyika katika ukumbi wa
uwanja wa ndani wa Taifa Mwankemwa atapanda ulingoni na Ramadhani
Shauri na Matumla atamkabili Seleiman Shabani Picha na SUPER D BOXING NEWS
………………………………………………………………………………
Na Mwandishi Wetu
Bondia Meshack Mwankemwa wa
Mbeya ameingia jijini Dar es salaam kwa ajili ya mpambano wake na
Ramadhani Shauri mpambano utakaokuwa wa raundi kumi za ubingwa wa EAST/
CENTRAL AFRICA siku ya Feb 5/ 2017 katika uwanja wa ndani wa Taifa .
Akizungumza na wahandishi wa
habari Promota wa mpambano huo Sadick Kinyogoli amesema kuwa huu ni
wakati wa mwisho wa kuelekea mpambano wenyewe utakaofanyika mwishoni
mwa wiki hii kwenye uwanjwa ndani wa Taifa.
Sadick Kinyogoli amesema
Mwankemwa ametua jijini tangu mwishoni mwa wiki iliyopita na Shauri ni
mkazi wa jiji la Dar es salaam kwa hiyo mpambano huo utakuwa mkali
sana kwa kuwa mabondia wote wameshacheza mapambano makubwa ya kimataifa
hivyo wapenzi wajiandae na kufika mapema ili kuangalia burudani ya
mchezo wa masumbwi waliyoikosa kwa kipindi kirefu.
Katika mpambano huo pia
kutakuwa na mapambano mengine ya kusindikiza mtanange huo ambapo
Kinyogoli ameongeza kuwa bondia Mohamed Matu, atapambana na Mfaume
Mfaume wakati bondia chipukizi anayekuja kwa kasi katika mchezo huu wa
masumbwi Iddi Mkwela ataonyeshana umwamba na Manyi Issa mpambano ambao
utakuwa na raundi kumi zisizokuwa na ubingwa
Mchezo mwingine wa ubingwa wa
taifa utakuwa kati ya Said Chino na Twalib Tuwa ubingwa wa taifa wa TPBC
mkanda ambao unatetewa na Tuwa Husein Pendeza wa Ashanti Boxing Clab
ya Ilala yeye atavaana na Said Hamdani kutoka Mbezi Conetion na Mbwana
Matumla atazichapa na Suleimani Shabani
Pamoja na mpambano hayo
kutakuwa na mpambano mwingine wa kimataifa kwa akina dada Anisha Bashir
kutoka Malawi na Ester Boazi Kazeba wa Tanzania
Kinyogoli ameongeza kwa kusema
kuwa mabondia wote watapima uzito pamoja na Afya zao siku ya Feb. 4/
2017 katika hotel ya Atrium iliyopo Sinza Afrika Sana hivyo mabondia
wote w
Tags
MICHEZO KITAIFA