BANDA MEDIA BLOG

MBUZI, NG'OMBE WASHIRIKI KUOMBEA MVUA

Na Peter Mkwavila,Dodoma.
WANYAMA wanaofungwa majumbani wakiwemo Ng’ombe,Kondoo na Mbuzi wamekuwa kivutio kikubwa katika maombi maalumu ya kuomba mvua yaliyofanywa na waumini wa dini ya kiislamu kata ya Chang’ombe ambayo yaliandaliwa na Baraza kuu la bakwata kata hiyo mjini humo.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na mjumbe wa baraza kuu la bakwata kata hiyo Ibrahim Maffita,alisema kuwa kitendo cha kuwashirikisha wanyama hao ni kama ishara ya kuwakilisha wezao ambao wanaoishi porini ukizingatia kuwa na wao wanahitaji kupata baraka ya mvua.

Akizungumza na BANDA BLOG mjumbe huyo wa Bakwata kata alisema kuwa kitendo cha kuwaleta wanyama ni ishara ya kuwawakiisha mbele za Mwenyezi Mungu ili kuwafanikisha kupata mahitaji wanayoyahitaji kama wanyama wa porini ambayo kwa kupitia mvua hiyo wanaweza kupata majani na maji.
Kwa upande wake Alhaji Omary Salumu akitoa hutuba yake kwa waumini hao kwenye ibada hiyo ya maombi,aliwataka kutumia fursa ya mvua zilizoaanza kunyesha kulima mazao yatakayokomaa haraka ambayo yatakostahimili kulingana na mvua zinazonyesha kwa mikoa ya kanda ya kati.
“Ndugu zangu waumini wa dini ninawaomba tutumie muda huu ambao mvua zimeanza kunyesha kwa kulima na kupanda mbegu itaayokomaa mapema,badala ya kuyaacha maji hayo yakipita bure ni vizuri basi yakatumika kwa kulima mazao ambayo yatakayokomaa mapema kwa ajili ya kupata chakula cha kutosha”alisema.
Naye Alhaji Husseni Jumbe ambaye ni Shekhe wa kata ya Chang’ombe aliwataka waumini kuendelea na moyo ya kupenda kufanya ibada mbele za mungu mara kwa mara,badala ya kusubiri mpaka majanga yatokee na ndipo waweze tukusanyika na kumlilia mwenyezi Mungu.
Alisema kuwa siyo tu wakati wa majanga ndipo waumini wakutanike na kuungana kwa pamoja juu ya kumlilia mungu,bali hata pale ambapo hakuna matatizo yoyote wanaweza kukutana kwa umoja na kuweza kumwomba na yeye akatubariki.
Hata hivyo Shekhe huyo aliwahimiza waumini kuwa na umoja na kutekeleza haki bila kujali imani ya mtu,kwa kuwa wakifanya hivyo Mungu atatuletea neema katika nchi yetu pamoja na ardhi ambayo tumepewa kwa ajili ya matumizi yanayostahili na kupendezwa na mungu mwenyewe.
Mwisho

Post a Comment

Previous Post Next Post
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG