BANDA MEDIA BLOG

FEZA NA TAASISI YA TIME TO HELP YAIPIGA TAFU S/M NIANJEMA


1
Mbunge wa jimbo Bagamoyo, dk. Shukuru Kawambwa, akishukuru baada ya shule ya msingi Nianjema kupokea madawati 60 kutoka kwa shule za Feza na wadau, taasisi ya Time To Help .
2
Mwalimu mkuu msaidizi wa shule ya msingi Nianjema, Bagamoyo, Ally Swalehe akipokea madawati 60 kutoka kwa mkurugenzi wa shule za Feza, Ibrahim Yunus.

3
Mkurugenzi wa shule za Feza Ibrahim Yunus akizungumza na walimu na wanafunzi wa shule ya msingi Nianjema na kabla ya kuwakabidhi madawati 60 aliyochangia kwa kushirikiana na taasisi ya Time To Help.
(picha na Mwamvua Mwinyi)
Na Mwamvua Mwinyi, Pwani
Mkurugenzi wa shule za Feza Ibrahim Yunus kwa kushirikiana na taasisi ya Time to Help wametoa msaada wa madawati 60 yenye yaliyogharimu mil. 10 kwa shule ya msingi Nianjema,Bagamoyo .
Akikabidhi madawati hayo,Yunus  alisema ,lengo ni kusaidia kukabiliana na changamoto ya upungufu wa madawati shuleni hapo.
Alisema pia yatawezesha kuondoa tatizo la kukaa chini kwa wanafunzi hao na kusoma katika mazingira bora.
Aidha Yunus alieleza kwamba kuanzia sasa shule za feza zitakuwa rafiki wa shule ya msingi Nianjema na kusaidia kusomesha wanafunzi watakaofaulu mitihani ya darasa la saba.
“Fanyeni kama ilivyo kwa shule zangu ambazo zimeongoza kwa kutoa mwanafunzi wa kwanza na kuwa shule ya kwanza kitaifa”
“Madawati haya wamechanga watu wa kawaida na kwa kushirikiana na shirika dada la Time To Help,naamini itakuwa chachu katika kuinua taaluma “alisema Yunus.
Katibu mkuu wa Time to Help, Ibrahim Ebrahim,alisema jukumu la kutatua changamoto za sekta ya elimu ni la jamii,wadau pasipo kuiachia serikali pekee.
Nae mbunge wa jimbo la Bagamoyo na Waziri wa zamani wa Elimu,dk Shukuru Kawambwa alishukuru kupata msaada huo .
Alisema madawati hayo 60 yatakaliwa na wanafunzi watatu kila dawati hivyo kuwaondolea adha wanafunzi 180 waliokuwa hawana madawati.
Dk Kawambwa alisema kuwa madawati hayo yatasaidia kuhakikisha wanafunzi wanakaa kwenye madawati ambapo wataweza kuandika vizuri.
Kaimu mwalimu mkuu wa shule hiyo Ally Swalehe alisema ,wanakabiliwa na upungufu wa madawati 287 huku shule hiyo ikiwa na wanafunzi 2,168 .
Alisema changamoto nyingine ni ongezeko la uandikishwaji wa wanafunzi kutokana na mfumo wa elimu bure ambapo uandikishaji umefikia asilimia 32 na kusababisha msongamano wa wanafunzi

Post a Comment

Previous Post Next Post
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG