Timu yaTaifa ya mpira wa miguu ya
Vijana wa Tanzania wenye umri wa chini ya miaka17 ‘Serengeti Boys’,
Jumamosi tarehe 04 Machi, 2017, watatembelea Kituo cha vijana
wanaopatiwa matibabu baada ya kuathirika na dawa za kulevya.
Kituo hicho kinachoitwa Sober
House kipo Bagamoyo mkoani Pwani. Ni kituo maalumu kwa tiba ya vijana
kinaendeshwa na kusimamiwa na Shirika la Life and Hope Rehabilitation
Centre chini ya Mkurugenzi, Al-Karim Bhanji.
Ikiwa huko, vijana wa Serengeti
Boys ambao kwa sasa wako kwenye kipindi cha mabadiliko ya katika sayansi
ya mwili hivyo itakuwa somo kubwa kwao katika kujielimisha kuhusu
mustakabali wamaisha yao.
Kwa upande wa TFF kuwapeleka vija
na hao huko ni utekelezaji Kanuniya 36 (7) ya Ligi Kuu ya Vodacom
inayozungumza kukataa rushwa, madawa, ubaguzi, fujo, kamari na mambo
mengine
Tags
MICHEZO KITAIFA