![]() | |
| WAZIRI wa nchi 0fisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma na utawala bora Anjelah Kairuki akiongea jambo kabla ya kuzindua rasmi ofisi yake mpya iliyopo Chuo kikuu cha Dodoma UDOM |
Waziri Kairuki wakifurahia Jambo pamoja na Katibu mkuu wa Wizara hiyo wakati Waziri huyo alipomtembelea Ofisini kwa katibu huyo [PICHA NA JOHN BANDA WA BANDA BLOG]
![]() |
| Waziri Kairuki, Katibu Mkuu wa wizara hiyo Dkt,Laurean Ndumbaro na Naibu Katibu Mkuu Susan Mlawi wakiwa katika picha ya pamoja mbele ya jengo la ofisi za Utumishi lililopo UDOM |
![]() |
| PICHA YA PAMOJA |
![]() |
| Prof Kikula akitoa ufafanuzi mbele ya waandishi wa habari kuhusu hisia kuwa kutakuwa na muingiliano chuoni hapo kati ya watumishi na wanafunzi |
Na John Banda, Dodoma
WAZIRI wa nchi 0fisi ya Rais Menejimenti ya utumishi
wa Umma na utawala bora Anjelah Kairuki amezindua rasmi utoaji wa huduma kwa
wananchi katika ofisi yake mpya iliiyopo chuo kikuu cha Dodoma Udom ambapo
jumla ya watu 17 tayari wameshapatiwa huduma toka januari 30 mwaka huu.
Akizungumza na waandishi wa habari pamoja na
watumishi wa wizara hiyo wakati wa zoezi la uzinduzi wa ofisi ya wizara hiyo
Kairuki alisema kuwa ni sehemu ya kuunga mkono agizo la serikali kuhamia
Dodoma.
Alisema kuwa ofisi hiyo ambayo ipo katika jengo la
ofisi ya shule ya Sanaa na sayansi za jamii katika chuo kikuu cha Dodoma Udom
na kuwataka wananchi wote wanaohitaji huduma yao kufika katika eneo hilo.
“Aidha napenda kutumia fursa hii kuwapongeza na
kuwashukuru wakala wa majengo TBA kwa kazi nzuri ya ukarabati na kuliweka jengo
letu katika hali nzuri kwa kipindi cha muda mfupi ambapo inawawezesha watumishi
kutoa huduma kama kawaida.
Aliongeza kuwa kutokana na uhamisho huo wa ofisi
masula yanayohusu sera na sheria za utumishi wa umma na utawala wa utumishi wa
umma ndiyo yatakayo tekelezwa katika ofisi ya Dodoma.
“Masuala ya usimamizi wa malipo ya mishahara,
uendeshaji rasilimaliwatu, ukuzaji maadili, anuai za jamii, uchambuzi ushauri
wa utendaji kazi na huduma ya teknolojia ya habari na mawasailiano
kushughulikiwa na ofisi yetu ya Dar es saaalam kwa sasa kwa kuwa idara hizo
zimepangwa kuhamia Dodoma katika awamu ya pili na tatu”alisema.
Naye makamu mkuu wa chuo kikuu cha Dodoma (Udom)
Prof, Idris Kikula alisema kuwa jumla ya wizara sita zinatarajiwa kuweka makazi
yake katika chuo hicho.
Kikula alisema kuwa haoni tatizo kwa serikali kuweka
makazi yake hapo wakati wakiendelea kujipanga kutafuta eneo ambalo litakuwa ni
la kudumu kwajili ya serikali tofauti na ambavyo watu wamekuwa wakisema katika
mitandao ya kijamii.
“Watu wanadai eti muingiliano wa watumishi na
serikali utaleta matukio ya vitendo vya umalaya lakini mimi kwangu naona huo ni
mtazamo hasi ambao hauna tija mbona Ifm, Udsm, Cbe, Mipango kunamuingiliano wa watu
na hakuna tabia hizo huwezi kuzuia munigiliano wa watu hata siku moja”alisema
Kikula.
Hatahivyo alizitaja wizara hizo ambazo zinatarajiwa
kuweka ofisi zake katika chuo hicho kuwa ni Katiba na sheria, Utumishi wa umma,
Viwanda na Biashara, Afya, Elimu pamoja na Wizara ya mambo ya ndani ya nchi.
Mwisho.
Tags
HABARI KITAIFA










