Chama cha Mapinduzi kimewafukuza makada 12 wa chama hicho wakiwemo
wanachama mkongwe kama, Sophia Simba, Ramadhan Madabida na Jesca
Msambatavangu.
Wakati wanachama hao wakifukuzwa wengine wanne wamepewa onyo kali, sita
wamevuliwa uongozi na kuwekwa chini ya uangalizi mkali wa miezi 30,
huku mwenyekiti wa chama hicho Dodoma, Adam Kimbisa akisamehewa.
Uamuzi huo umetolewa baada wa kikao cha Nec kilichofanyika Dodoma leo
(Jumamosi) na kuongozwa na mwenyekiti wake, Rais John Magufuli.
Tags
CCM