Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa
akizungumza na Waziri wa Mambo ya Nje wa Mauritius, Bw. Vishnu
Lutchmeenaraidoo baada ya kuwasili kwenye uwanja wa ndege wa Kimataifa
wa Sir Seewoosagur Ramgoolam nchini Mauritius kumwakilisha Rais John
Pombe Magufuli katika Uzinduzi wa Jukwaa la Uchumi la Africa mjini Port
Luis kuanzi Machi 20, 2017. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa
akizungumza na Waziri wa Mambo ya Nje wa Mauritius, Bw. Vishnu
Lutchmeenaraidoo baada ya kuwasili kwenye uwanja wa ndege wa Kimataifa
wa Sir Seewoosagur Ramgoolam nchini Mauritius kumwakilisha Rais John
Pombe Magufuli katika Uzinduzi wa Jukwaa la Uchumi la Africa mjini Port
Luis kuanzi Machi 20, 2017. Kulia ni mkewe Mary.(Picha na Ofisi ya
Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa
akizungumza na Waziri wa Mambo ya Nje wa Mauritius, Bw. Vishnu
Lutchmeenaraidoo baada ya kuwasili kwenye uwanja wa ndege wa Kimataifa
wa Sir Seewoosagur Ramgoolam nchini Mauritius kumwakilisha Rais John
Pombe Magufuli katika Uzinduzi wa Jukwaa la Uchumi la Africa mjini Port
Luis kuanzi Machi 20, 2017. Kulia ni mkewe Mary.(Picha na Ofisi ya
Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa
akiogozwa na Waziri wa Mambo ya Nje wa Mauritius, Bw. Vishnu
Lutchmeenaraidoo wakati alipopokelewa kwenye uwanja wa ndege wa
Kimataifa wa Sir Seewoosagur Ramgoolam nchini Mauritius kumwakilisha
Rais John Pombe Magufuli katika Uzinduzi wa Jukwaa la Uchumi la Africa
mjini Port Luis kuanzi Machi 20, 2017. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
………………………………………………………………………
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa
amewasili nchini Mauritius leo (Jumapili, Machi 19, 2017) kwa ajili ya
kumuwakilisha Mheshimiwa Rais Dkt. John Magufuli katika mkutano wa
kuzindua Jukwaa la Uchumi Barani Afrika (AEP).
Kwenye uwanja wa ndege wa
Kimataifa wa Sir Seewoosagur Ramgoolam Waziri Mkuu amepokelewa na Waziri
wa Mambo ya Nje wa Mauritius Mheshimiwa Vishnu Lutchmeenaraidoo.
Uzinduzi wa jukwaa hilo
unatarajiwa kufanyika kesho mjini Port Louis ambapo utawakutanisha
viongozi wakuu wa nchi za Afrika, wanazuoni, wafanyabiashara pamoja na
watu kutoka kwenye asasi mbalimbali za kiraia barani Afrika.
Pamoja na kuhudhuria mkutano huo,
pia Waziri Mkuu ambaye ameambatana na mkewe Mama Mary Majaliwa
anatarajiwa kuwa mgeni rasmi kwenye Kongamano la Biashara kati ya
Tanzania na Mauritius litakalofanyika Machi 23, 2017.
Aidha, Waziri Mkuu mara baada ya
kumaliza mkutano huo anatarajia kutembelea maeneo maalumu ya uwekezaji,
viwanda vya sukari na nguo.
Waziri Mkuu ameambatana na Waziri
wa Fedha na Mipango wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar,Dkt. Khalid Salum
Mohammed na Waziri wa Viwanda na Biashara, Mheshimiwa . Charles Mwijage
pamoja na maofisa wengine wa Serikali.
Tags
UCHUMI / BIASHARA