Mmoja wa wakufunzi wa mafunzo kwa wanahabari kutoka mikoa ya Kanda ya Ziwa ambayo ni Mwanza, Mara, Geita na Simiyu, Marie Engel, akiwasilisha mada kuhusu umuhimu wa kuandika habari juu ya Haki za Binadamu hususani za kiafya.
#BMGHabari
Mafunzo
hayo ya siku mbili tangu jana, yameandaliwa na Taasisi ya Vyombo vya
Habari Kusini mwa Afrika (MISA) Tawi la Tanzania, yakilenga kuwajengea
wanahabari uelewa juu ya Sheria
Mpya ya Huduma za Habari ya mwaka 2016 na Kanuni zake za mwaka 2017 ili
kuwasaidia katika utendaji wa majukumu yao bila kukinzana na sheria na
kanuni hizo.
Pamoja
na mambo mengine, washiriki wa mafunzo hayo yaliyofadhiliwa na Taasisi
ya Friedrick Ebert Stiftung (FES) Tanzania, wamefundishwa sheria na
taratibu za kuandika na kuripoti habari/ makala kuhusu haki za binadamu
kwa kuangazia sekta ya afya juu ya habari na makala za magonjwa ya
kuambukiza kama HIV/Ukimwi ambapo wameahidi kuifikisha elimu hiyo kwa
wenzao na pia kuitumia vyema katika kuboresha utendaji kazi wao.
Wanahabari
washiriki wa mafunzo hayo wakifuatilia mada kutoka kwa mkufunzi Marie
Engel, kutoka shirika la Umoja wa Mataifa UNAIDS nchini Tanzania.
Baadhi
ya washiriki wa mafunzo hayo. Aliyesimama ni Afisa Habari na Utafiti
kutoka Taasisi ya Vyombo vya Habari Kusini mwa Afrika (MISA) tawi la
Tanzania, Gasirigwa Sengiyumva.
Mwakilishi wa Metro Fm Mwanza, Alphonce Kapela, akichangia mada kwenye mafunzo hayo
Sehemu ya washiriki wa mafunzo hayo
Mafunzo yakiendelea
Mafunzo kwa vitendo yakiendelea nje ya ukumbi
Hii inaitwa noa bongo, ukirushiwa mpira unaeleza ulichojifunza kwenye mafunzo hayo
Mafunzo nje ya ukumbi yakiendelea
Mmoja wa wakufunzi wa mafunzo hayo, Wakili James Marenga, akisimamia zoezi hilo
Afisa
Habari na Utafiti kutoka Taasisi ya Vyombo vya Habari Kusini mwa Afrika
(MISA) tawi la Tanzania, Gasirigwa Sengiyumva, akiteta jambo na mmoja
wa wakufunzi wa mafunzo hayo, Marie Engel, kutoka shirika la Umoja wa Mataifa UNAIDS nchini Tanzania.
Picha
ya pamoja, waandaaji wa mafunzo, wakufunzi wa mafunzo pamoja na
washiriki wa mafunzo ambao ni wanahabari kutoka mikoa ya Kanda ya Ziwa
ambayo ni Mwanza, Mara, Geita na Simiyu.
Tags
HABARI KITAIFA