![]() |
| Watoto wakitafuta uwezekano wa kupita katika eneo hilo ambalo kwa asili ni eneo lenye tope jingi |
WAKAZI wa mtaa wa senje kata ya msalato manispaa ya
Dodoma wameshangazwa na taarifa ya matengenezo ya barabara yenye ulefu wa km 1
katika mtaa wao toka manispaa huku wao wakiendelea kupata adha ya kushindwa
kuitumia katika misimu yote ya mvua kutokana na ubovu
Akiongea na waandishi wa habari mzee Yona Mkuki ambae
ni mkazi wa miaka mingi katika mtaa huo alisema kuwa Barabara hiyo haijawahi
kuonja greda tangu mwaka 1979 ilipochongwa na jeshi.
Mkuki alisema baada ya hapo hakujawa na chombo au
mtu toka manispaa aliyefika na kufanya matengenezo yoyote pamaoja na kuwa kila
mtu anajua adha wanayoipata ya magari kushindwa kupita hali inayowasababishia
wagonjwa kutembea kwa miguu na wengine kubebwa migoni mpaka kufika kuliko na
unafuu
“taarifa ya barabara hii kutengenezwa mwaka jana
ndiyo nazisikia sasa hivi labda kama kule ofisini na kwenye makaratasi yao
lakini kiuhalisia tunapata adha kubwa kutokana na mashimo yanayosabisha maji
kutuama tena kukiwa na tope jingi wakati wa mvua
Mwaka jana sina niliyemuona wala greda bali
ninachojua barabara hii ilitengenezwa na jeshi mwaka 1979 alisema”,
Kwa upande wake Diwani wa Kata ya Msalato Ally
Mdende Mohamed alisema mwanzoni mwa mwaka 2016 aliomba kutengenezewa barabara
hiyo na baadae ikaingizwa kwenye mpango wa kutengenezwa baada ya mhandisi kufanya
savei
Diwani huyo alisema kuwa kilichomshangaza ni mwezi
octoba mwaka jana kuona kwenye makablasha kuwa barabara hiyo ilishatengenezwa
na mkandarasi Alishalipwa fedha yote zaidi ya 8.6 mil
“Hii ni ajali niliyokuwa nimetegeshewa ili nije
kuonekana kuwa nimepewa fedha na kuzila mimi na huyo mkandarasi kitu ambacho
mimi sikuhusika
Aidha alisema kablasha linaonyesha kuwa barabara
hiyo imechongwa na kushindiliwa, karavati limejengwa, vichaka vimefyekwa na
visiki kung’olewa kitu ambacho siyo cha kweli
Tags
MRADI HEWA




