Diwani
wa kata ya Pangani,Agustino Mdachi akizungumza na wananchi wa kata hiyo
kwenye ziara ya mbunge wa jimbo la Kibaha Mji,Silvestry Koka
aliyoifanya katika kata hiyo.
Baadhi
ya wakazi wa kata ya Pangani,wakisikiliza jambo katika ziara ya mbunge
wa jimbo la Mji wa Kibaha, Silvestry Koka kwenye kata hiyo.
Mbunge wa jimbo la Mji wa Kibaha ,Silvestry Koka,akizungumza jambo katika ziara yake kata ya Pangani .(picha na Mwamvua Mwinyi).
……………
Na Mwamvua Mwinyi,Kibaha
WANAFUNZI
wa shule ya sekondari ya kata ya Pangani,Kibaha Mji,wanakabiliwa na
adha ya kutembea umbali wa km.34 kila siku,hali inayosababisha baadhi
yao kuwa watoro, kukatisha masomo na kupata mimba.
Aidha
shule za msingi zilizopo katika kata hiyo,zina uhaba wa walimu ambapo
shule yenye wanafunzi 950 ina walimu kumi pekee hivyo kusababisha muda
mwingi wanafunzi kucheza.
Hayo
aliyasema diwani wa kata ya Pangani,Agustino Mdachi,wakati alipokuwa
akizungumzia changamoto za kielimu ,kwenye ziara ya mbunge wa jimbo la
Mji wa Kibaha,Silvestry Koka,aliyoifanya katika kata hiyo.
Alisema,wanafunzi wanaosoma kwenye ya shule ya kata wanapata usumbufu na wapo katika wakati mgumu.
Mdachi
alieleza kwamba,hakuna usafiri wa daladala zaidi ya kutumia miguu na
pikipiki ambazo wanalipa 10,000 hivyo kusababisha wanafunzi hasa wa kike
kurubuniwa na madereva bodaboda na kupata mimba.
“Watoto wetu huku hawamalizi shule ya sekondari,ni watoro,wanakatiza masomo na wengine wakipewa mimba ,hii inatokana na shule yetu ya kata kuwa mbali”alisema Mdachi.
Akizungumzia tatizo la upungufu wa walimu katika shule za msingi ,alisema shule ya msingi kama Lumumba na Kidimu zina wanafunzi zaidi ya 900 na walimu ni 10 pekee hivyo watoto wengi wanacheza ,hawafundishi na kufeli.
“Watoto wetu huku hawamalizi shule ya sekondari,ni watoro,wanakatiza masomo na wengine wakipewa mimba ,hii inatokana na shule yetu ya kata kuwa mbali”alisema Mdachi.
Akizungumzia tatizo la upungufu wa walimu katika shule za msingi ,alisema shule ya msingi kama Lumumba na Kidimu zina wanafunzi zaidi ya 900 na walimu ni 10 pekee hivyo watoto wengi wanacheza ,hawafundishi na kufeli.
Nae
mbunge wa jimbo la Mji wa Kibaha,Koka amemuagiza diwani na kamati ya
maendeleo kata,kuandika barua ambayo ataisaini na kisha ipelekwe kwa
mkurugenzi kuhakikisha anaongeza walimu katika shule hizo.
Alitoa
siku 30 kwa mkurugenzi wa halmashauri ya mji huo,kushughulikia suala
hilo kwa kuangalia taratibu zinazotakiwa kufuata ili kupeleka walimu
watakaosaidia kupunguza adha hiyo.
Koka alifafanua,yawekwe mazingira bora kwa wanafunzi ikwemo kuongeza walimu wa kutosha ,kama ilivyo kwa shule za Mailmoja ambako shule moja ina wanafunzi 500 na walimu 30.
Alimtaka mratibu wa elimu kata na idara ya elimu halmashauri ya mji wa Kibaha kusimamia changamoto hiyo kwa kushirikiana na mkurugenzi na kupanga walimu kwa uwiano .
Koka alifafanua,yawekwe mazingira bora kwa wanafunzi ikwemo kuongeza walimu wa kutosha ,kama ilivyo kwa shule za Mailmoja ambako shule moja ina wanafunzi 500 na walimu 30.
Alimtaka mratibu wa elimu kata na idara ya elimu halmashauri ya mji wa Kibaha kusimamia changamoto hiyo kwa kushirikiana na mkurugenzi na kupanga walimu kwa uwiano .
Koka
alieleza suala la kutembea umbali mrefu linaumiza watoto,hivyo ingaliwe
namna ya kutafuta eneo mtaa wa Kidimu ili jamii ianze kujitolea kujenga
shule nyingine na yeye ataongeza nguvu zake.
Tags
ELIMU