Frank Mvungi-Maelezo
Serikali imewataka Wananchi
kushiriki Kutunza Mali Kale kwa Faida ya Kizazi hiki na Kizazi kijacho
ili ziweze kuchangia katika Kukuza Uchumi.
Kauli hiyo imetolewa na
Mkurugenzi wa Mambo ya Kale toka Wizara ya Mali Asili na Utalii Dkt.
Donatius Kamamba wakati wa mkutano na waandishi wa habari uliolenga
kuhamasisha wananchi kutumia fursa zinazotokana na uwepo wa mali kale.
leo Jijini Dar es Salaam.
“Mali Kale ni kichocheo cha
Utalii na ukuaji wa Uchumi hapa nchini hivyo ni muhimu zikatunzwa na
kuenziwa ili ziweze kusaidia Taifa kukuza sekta ya Utalii nchini”
Alisisitiza Dkt. Kamamba.
Akifafanua zaidi Dkt. Kamamba
amesema kuwa Mali kale ni urithi wa taifa na sekta hiyo imekuwa
ikichochea Tafiti,machapisho na makala simulizi hivyo kuchochea ukuaji
wa sekta ya elimu na uchumi kwa ujumla.
Kwa upande wake Mwakilishi wa
Mkurugenzi Msaidizi utafiti Dkt.Emmanuel Bwasiri amesema kuwa mali kale
ni utambulisho wa taifa letu hivyo ni muhimu kusaidia katika kutunza
rasilimali hizo ambazo zinasaidia kwa kiwango kikubwa kukuza uchumi.
Akizungumzia vigezo vinavyotumika
kutangaza eneo kuwa urithi wa taifa Dkt Bwasiri amesema kuwa ni Sifa ya
Kiuchumi,Kijamii,Kielimu na Kihistoria.
Serikali imekuwa ikisisitiza utunzanji wa Mali kale katika maeneo mbalimbali hapa nchini ili ziweze kuchochea ukuaji wa uchumi.
Tags
MALIASILI/UTALII