Meneja Masoko
la Mawasiliano wa LAPF, James Mlowe (katikati), akizungumza katika
mkutano na wanahabari Dar es Salaam leo, kuhusu mkutano wa tisa wa LAPF
utakaofanyika Machi 9 na 10, 2017 Ukumbi wa Mikutano ya Kimataifa wa
AICC jijini Arusha. Kulia ni Meneja wa Takwimu Hadhari na Tathmini wa LAPF, Abubakar Ndwata na Ofisa Masoko na Mawasiliano wa LAPF, Rehema Mkamba.
Meneja wa Takwimu Hadhari na Tathmini wa LAPF, Abubakar Ndwata (kulia), akizungumza kwenye mkutano huo. Kushoto ni Meneja Masoko la Mawasiliano wa LAPF, James Mlowe.
Wapiga picha wakichukua taarifa hiyo.
………………………………………………………………
Mfuko wa Pensheni wa LAPF
unatarajia kufanya mkutano wa tisa wa wadau tarehe 9 na 10 Machi, 2017
katika ukumbi wa mikutano wa kimataifa wa AICC Jijini Arusha. Mgeni
rasmi katika mkutano huu anatarajiwa kuwa Waziri mkuu wa jamhuri ya
muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa(Mb).
LAPF imekuwa ikifanya mikutano
hii ili kutoa taarifa za undeshaji wa Mfuko na kuwapa fursa wadau kutoa
maoni mbali mbali ili kuboresha utendaji wa Mfuko. Aidha mikutano hii
hufanyika ili kutekeleza maagizo ya mamlaka ya usimamizi na udhibiti wa
mifuko ya Hifadhi ya jamii nchini (SSRA).
Kauli mbiu ya mkutano wa mwaka
huu ni “Kuibua Fursa Endelevu za Ajira kwa maendeleo ya Hifadhi ya Jamii
Tanzania”. Pamoja na mambo mengine kwenye mkutano huu mada mbali mbali
zitawasilishwa ikiwemo mada inayohusu kauli mbiu jatwa hapo juu. Mada
nyingine zitahusu Utendaji wa Mfuko kwa kipindi cha mwaka wa fedha
2015/2016, Taarifa ya uwekezaji pamoja na Taarifa ya Hesabu za Mfuko kwa
mwaka 2015/2016.
Kadhalika katika siku ya kwanza
ya ufunguzi wa mkutano LAPF itazindua huduma ya Mkopo wa Kujikimu
ijulikanayo kwa jina la Maisha Popote na LAPF) kwa kushirikiana na benki
ya CRDB. Huduma hii imewanufaisha sana wanachama wa Mfuko wanaoanza
ajira kwa kuwapa fursa ya kukopa mara tatu ya mshahara wao ili kukidhi
mahitaji ya awali kama kulipa pango, nk kwa riba nafuu.
Vilevilesiku ya ufunguzi wa
mkutano tarehe 09 Machi, 2017 itakuwa ni siku ya maadhimisho ya figo
duniani hivyo basi LAPF itatumia siku hii kuwapa fursa wadau wote
watakao shiriki mkutano huu kupima figo kwa kushirikiana na wataalamu
kutoka hospitali ya KCMC.
LAPF inatarajia kupata washiriki
zaidi ya 600 katika mkutano huu kwa kuzingatia idadi ya waalikwa.
Waalikwa wanaweza kuthibitisha ushiriki wao na kujisajili kwa kutembelea
tovuti ya Mfuko www.lapf.or.tz . LAPF inawahamasisha wadau wote kujisajili kupitia tovuti ili kupunguza msongamano siku ya mkutano.
Aidha,siku ya pili ya mkutano
tarehe 10 Machi, 2017, LAPF pamoja na washiriki wote wa mkutano
wakiongozwa na Waziri Mkuu, Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa wanatarajia
kushiriki katika mazoezi ya kutembea ikiwa ni kuunga mkono utekelezaji
wa tamko la Makamu wa Rais, Mh. Samia Suluhu Hassan.
Karibuni waalikwa wote kwa ustawi wa Mfuko.
Staafu kwa Ufahari na LAPF.
Tags
HABARI KITAIFA