Kamati ya Maadili ya TFF imemsimamisha Mkuu wa Idara ya Habari na
Mawasiliano wa Simba SC, Haji Manara kujihusisha na soka ndani na nje
kwa muda wa miezi 12 na faini shilingi milioni 9 vyote kwa pamoja
Mapema wiki hii TFF ilimfungulia mashtaka Manara kwenye Kamati hiyo
inayoongozwa na Wakili Jorome Msemwa kutokana na kauli alizotoa wakati
wa mkutano wake na waandishi wa habari makao makuu ya klabu ya Simba SC.
