Kwanza niseme nawapenda sana, nawashukuru sana kwa mapokezi makubwa
mliyonipa, Kilichinitoa machozi ni heshma kubwa mliyonipa kina mama.
Mlilala chini, mkataka nipite juu yenu, sio jambo ambalo nilitegemea,
nawashukuru sana. Niwaahidi nitafanya kazi kwa nguvu zangu zote,
kuwatumikieni, usiku na mchana, ntaikumbuka heshima mliyonipa na hio
itanisukumu.
Mmenipa heshima kubwa mpaka ntaenda nayo kaburini, pengine sikustahili,
upendo wenu umegusa sana moyo wangu. Ntatumia mpaka senti yangu ya
mwisho kuhakikisha jimbo la Mtama lina maisha bora. Niwashukuru Steve
Nyerere na kundi lake, waandishi wa habari leo wote wamekuja Mtama.
Nilitaka kuongea Dar es Salaam, ikatokea fujo kidogo, Nimeamua kuja nyumbani na leo nitasema.
Mimi ni mtoto wa Kimakonde na nimefundishwa kusema kweli, nimshukuru
Rais ambae nilipigana kufa na kupona kuhakikisha anakuwa Rais, nilipata
ajali mabya usiku wa manane wakati natoka kutafuta kura. Watanzania
wakatupa dhamana na nikapata heshma ya kuwa kwenye baraza la mawaziri
moja kwa moja bila kuwa naibu waziri.
Sina mashaka kuwa nilifanya kazi nzuri kwa akili yangu yote kuhakikisha
dhamana niliyopewa nameifanyia haki, kama yupo anadhani sikutenda haki
asimame hadaharani. Wakati nateuliwa hakukuwa na majadiliano.
Karatasi ukiisoma haina sababu, yalikuwa ni mabadiliko ya kawaida
kulingana na Rais. Wakati mwingine ukiwa na mchezaji mahiri na mkafunga
magoli ya kutosha, mnampumzisha akacheze tena kesho.
Siku nne au tano kabla ya mabadiliko nilisema mambo kama hayaendi sawa
mimi ntajiuzulu. Nilisema kazi hii ngumu na ikithibitika amevamia kituo
cha habari, mimi waziri sitatakiwa kubaki madarakani, watu tunatakiwa
kuishi kwenye maneno yetu, mimi no mtoto wa mzee Nnauye, ukifika mahali
usiyombishwe na cheo.
Kocha ameamua, hakuna sababu ya kumnunia, mechi ikikamata ntarudishwa uwanjani, mimi ni mchezaji bora.
Kwenye sakata hilo kuna mambo ya kipuuzi, haya nitasema. Nikiwa njiani
kurudi kutoka Arusha, kuna watu walisema kwenye mitandao Nape
amekamatwa, baada ya kukanusha wakaenda kuwaondoa waandishi wa habari
hoteleni.
Nilipofika nikakuta waandishi wa habari wamefukuzwa hotelini kwa ubabe,
wakaenda nje na mwenye hoteli abaki na hoteli yake. Wakamwaga vijana
wengi, nikisema vijana mnawajua. Mimi ninajua, nimekaa miaka 16 ndani ya
CCM na nilijua kilichokua kinaendelea na bahati nzuri wanahabari
wakaonyesha lile tukio live.
Nilivyofika nikawaona wale vijana, yule kijana mliemuona mpuuzi,
akasogea karibu yangu, nikamnong'oneza tuko moja kwa moja vyombo
vinaangalia, nikafikiri wana akili, nilisema kulinda sura ya nchi yangu,
vyombo vya Dola na Rais wangu. Nilikuwa nasitiri nchi yangu, mpuuzi
haoni, nikamwambia niliyonayo ni kubwa kuliko yako, sema nikaona wote
tutakuwa wapuuzi.
Nikaingia ndani ya gari na kutoka juu ili aje, ilihitaji busara na
nikiwaambia sina nia mbaya. Sikuwa na haja kuharibu kazi ya mikono yangu
mwenyewe.
Hivi nani aliweka mguu, Edward asiende mbele? Wao walikuwa kwenye meza
ndefu wanakunywa bia wakati wengine tunatafuta kura ndio maana
nilikasirika na naamini mtanisamehe kwa kukasirika kwango, mimi ni
banadaamu na nina nyongo, nilikumbuka mengi sana.
Kitenndo kilichofanyika hakikuwa cha kiungwana na namshukuru waziri wa mambo ya ndani kusema sina rekodi ya uhalifu.
Nilisubiri wamtafute, na wanasema sio polisi, leo nyoosha bastola hewani
uone kama polisi hawajaondoka na wewe na pale alikuwepo RPC.
Siamini kama alitumwa kuonyesha silaha, mimi ukinitolea silaha naoa kama
mic tu. Shida niliyonayo huyu jambazi alietoa silaha, vyombo vya ulinzi
na usalama vinafanya nae nini. Kama wameweza kumfanyia Nape, watanzania
wangapi watafanyiwa huku mitaani. Vingenevyo wataonewa wengi, naamini
wako wengi wametolewa huko, Kijana mmoja wa CHADEMA, Ben Saanane
amepotea kwa miezi mingi, watu wamevamia kituo na wameonekana, tusema
alieonekana sie yeye, nani alieagiza mtu akiwa na vyombo vya ulinzi na
usalama kuvamia studio. Matukio haya yanawafanya watu waishi kwa hofu
Dar imevamiwa studio akiwemo Roma Mkatoliki, sikwenda CCM kwa sababu
mzee Nnauye yuko CCM, nilienda CCM kwa sababu ya imani ilikuwa CCM, sema
kweli fitna kwangu mwiko.
Kazi ya msingi ya kikatiba ya serikali, ni kulinda raia na mali zao,
ombi langu kwa serikali na Rais aunde tume huru iyachunguze matendo haya
ili yasijirudie tena. Mimi nimewasemehe ila haya matendo mengine,
yanamjengea chuki yeye(Rais) na wananchi kwa sababu wanadhani ni yeye
ndie anaewatuma.
Matendo haya yanachonganisha CCM na wananchi, huko mtaani watu wanasema,
namshauri kama mwenyekiti wa chama changu, watu wachche wanaotumia
mamlaka waliyopewa kuumiza watu, lazima tume iiundwe.
Tags
Nape Nnauye
