Haya mambo bado yanachanganya wengi kwamba roho inaenda wapi baada ya kuachana na mwili
1.Je inaenda kuzimu?
2.Je inaenda peponi?
3.Je inazaliwa upya?
Maswali yote hapo juu yana majibu yanayofanana, kuwa roho zipo na
zinakuwa kote huko kulikotajwa kutegemeana na kwenye uhai wake kidunia
zilibeba/ zilifanya nini? Hebu twende moja baada ya jingine.
Kwanza, dini zote zinahimiza matendo mema na maisha baada ya kifo; hata
wapagani pia. Hivyo basi, japokuwa maelezo yanatofautiana, lakini msingi
unabaki kuwa ule ule wa roho kuwa sehemu husika.
1.Je, roho inaenda kuzimu? Jibu ni ndio
Kwamba bila kujali unaamini nini lakini jehanam iko hapahapa duniani ,
roho iliyotenda mabaya duniani baada ya kutoka katika mwili uharibikao
huingia kwenye mwili mwingine uliojaa mateso tabu na mahangaiko mengi!
Kumbuka ili roho iweze kubeba hisia za mateso na maumivu lazima zipate
jumba/ mwili!! Hiyo ni jehanam au kuzimu.
2.Je, roho huenda peponi? Jibu ni ndio
Pepo iko hapahapa duniani, roho iliyoishi kwa kutenda mema hubaki mahali
kwenye dunia hii ikiwa iko live lakini domant ikiwa haihisi wala
kufanya chochote na kama ikibidi kupata mwili huingia kwenye mwili ambao
haujui shida za dunia hii kila kitu kwake ni mteremko tu mpaka mwili
husika unapochoka na kuharibika/ kufa!! Hii ni peponi.
3.Je, roho inazaliwa upya? Jibu ni ndio japo kimsingi sio kuzaliwa upya
bali ni kupata makao/ makazi mapya hapa ndio penye dhana nzima ya
reincarnation, ambapo sasa hutegemea matendo ya nyuma Kwahiyo yaweza
kuwa kwenye mwili mzuri au mbaya refer pepo na kuzimu.
4.Je, roho zinatangatanga? Jibu ni ndio
kwanza roho huwa hazifi bali kuna wakati hukosa makao mapya/mwili baada ya zamani kwisha na kuharibika
Haijulikani hasa nini hutokea lakini hizi ni roho zenye matatizo makubwa
na ndio hizi huwa mashetani majini vinyamkera na viumbe vya ajabu
ajabu. Ni roho hizi hizi ambazo huweza kuingia kwenye familia kikundi au
mkusanyiko wowote na kuleta mirafaruku mikubwa tu ambayo mingine huleta
maafa makubwa.
Kwahiyo roho zipo na zipo sana na kamwe hazifi wala hazipotei jehanam,
na pepo zao zipo hapahapa duniani na kwenye kila nyanja ya maisha yetu
