|
|||
Mwenyekiti wa Bodi ya Hospitali ya
Taifa Muhimbili (MNH), Profesa Charles Majinge akizungumza katika
warsha kuhusu upasuaji wa matundu madogo bila kufungua tumbo
iliyofanyika kwenye hospitali hiyo leo. Daktari bingwa aliyebobea katika
upasuaji huo, Profesor Rafique Parkar kutoka Kenya ni mmoja wa watoa
mada kwenye warsha hiyo ambayo imeandaliwa na MNH. Watoa mada wengine ni
Dk Vicenti Tarimo wa Muhimbili, Dk. Abidan Mganga na Dk. Paul Kissanga.
Baadhi ya washiriki wakifuatilia warsha hiyo.
Mkurugenzi
Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Profesa Lawrence Museru
akiwakaribisha madaktari kutoka katika hospitali mbalimbali nchini.
Madaktari kutoka Hospitali ya Regency, Hospitali ya Seliani, Hospitali
ya Temeke na Hospitali ya Amana.
Washiriki wakifuatilia warsha leo ambayo imefanyika kwenye Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH).
Dk. Vicenti Tarimo wa Muhimbili akitoa mada kwenye warsha hiyo leo.
Baadhi
ya washiriki akiwamo Profesa Rafique Parkar , Profesa Charles Majinge
(kutoka kushoto) wakimsikiliza Dk. Vicent Tarimo wakati akitoa mada leo
kwenye warsha hiyo.
Washiriki wakiwa kwenye picha ya pamoja.
Tags
AFYA
