BANDA MEDIA BLOG

YANGA YAITANDIKA AZAM FC NA KUONGOZA LIGI KUU TANZANIA BARA


SD
Na.Alex Mathias,Dar es salaam.
Mabingwa watetezi wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania bara timu ya Yanga imerudi kwenye mbio za ubingwa baada ya kulipa kisasi kwa Azam FC cha bao 1-0 mchezo uliochezwa kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.

Yanga wakicheza bila ya nyota wake watano ambao ni Yondani,Kessy,Kamusoko,Tambwe na Ngoma huku Azam ikiwakosa Agrey,Kapombe na Bocco timu hizo zilianza kushambuliana kipindi cha kwanza huku Wana rambaramba wakionekana kuutawala Mchezo na kukosa nafasi nyingi za wasi.
Yanga imeendelea kupata rundo la majeruhi baada ya kiungo mkabaji wao Justine Zulu kuumia kwa mguu wa kushoto na kupelekea kukimbizwa Hospitali dakika ya 30 kwa kuchezewa madhambi na Himid Mao wakati akijiandaa kupiga Mpira katika eneo la Azam na nafasi yake kuchukuliwa na Emmanuel Martin.
Azam FC waliendelea kulishambulia lango la Yanga huku wachezaji wake kukosa umakini wa kumalizia nafasi ambazo walizipata na dakika ya 43 Mshambuliaji wa Azam Yahya Mohammed aliumia kwa kubanwa na msuli hivyo kushindwa kuendelea na nafasi yake kuchukuliwa na Mghana mwenzake Samuel Afful hadi mapumziko timu zilikuwa nguvu sawa.
Kipindi cha pili kilianza kwa timu zote kufanya mabadiliko na kuanza kushambuliana kwa zamu huku Yanga wakiingia kwa kucheza kimbinu zaidi kwa lengo la kupata pointi tatu Muhimu na katika dakika ya 70 Mzambia Obrey Chirwa aliwanyanyua mashabiki wa wake pamoja na benchi la ufundi baada ya kumtoka beki wa Azam FC, Yakubu Mohamed kufuatia pasi ndefu ya kiungo mchezeshaji, Haruna Niyonzima.
Kwa Matokeo hayo Yanga imeongoza Ligi kwa muda baada ya kufikisha jumla ya pointi 56 na nafasi ya pili ikishikwa na mahasimu wao Simba wenye pointi 55 na kesho watashuka dimbani kucheza na Kagera Sugar Mjini Bukoba na kuendelea kufukuzana kwenye mbio za Ubingwa.
Baada ya Mpira kumalizika FULLSHANGWEBLOG.COM ilifuatilia ili kujua hali ya Justine Zulu ambaye alikimbizwa Hospital na kupata taarifa kuwa Mchezaji huyu ameshonwa nyuzi tisa kwenye Mguu wake na kuweza kuongeza idadi ya majeruhi katika kikosi cha Yanga ambacho kinajiandaa na mchezo wa kombe la shirikisho dhidi ya MC Alger mwishoni mwa wiki inayokuja
Vikosi Yanga ; Deo Munishi ‘Dida’, Juma Abdul, Mwinyi Mngwali, Vincent Bossou, Nadir Haroub ‘Cannavaro’, Said Juma ‘Makapu’, Simon Msuva/Juma Mahadhi , Justin Zulu/Emmanuel Martin , Obrey Chirwa, Deus Kaseke/Geoffrey Mwashiuya  na Haruna Niyonzima.
Azam; Aishi Manula, Erasto Nyoni, Gardiel Michael, Daniel Amoah, Yakubu Mohammed, Himid Mao, Salum Abubakar ‘Sure Boy’, Frank Domayo, Yahya Mohmmed/Samuel Afful , Shaaban Iddi/Bruce Kangwa  na Ramadhani Singano ‘Messi’/Joseph Mahundi .

Post a Comment

Previous Post Next Post
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG