BANDA MEDIA BLOG

SASA WAZALISHAJI [WAKUNGA] KUTOA MAELEZO KIKITOKEA KIFO CHA MAMA AU MTOTO WAKATI WA KUJIFUNGUA

Makamu wa Rais akisisitiza jambo wakati alipokuwa akiongea na Wakunga, siku ya kilele cha maadhimisho ya wakunga Duniaani yaliyofanyika mjini Dodoma
Mtendaji Mkuu wa UNFPA Dkt, Hashina Begum akiongea jambo katika maadhimisho ya Kilele Cha siku ya Mkunga Duniani iliyofanyika mjini Dodoma  Mei 5,2017
Wauguzi na Wakunga Toka Mikoa mbalimbali kwa mamia wakiwa katika ukumbi wa Mwalimu Nyerere uliyopo Chuo Cha Mipango na Maendeleo Vijijini cha Mjini Dodoma wakati wa maadhimisho ya Siku ya Mkunga Duniani Iliyofanyika mjini Humo

Waliokaa Mbele ni Wakuu wa Wilaya za Chamwino, Mpwapwa, Dodma Mjini, Bahi na Chemba wakifurahia jambo  walipokuwa wakifuatilia Burudani ya Ngoma iliyokuwa ikitolewa na kundi la ngoma la mwinamila, wakati Maadhimisho ya Kilele cha Siku ya Wakunga Duniani iliyofanyika mkoani humo [PICHA NA JOHN BANDA]
Mkunga Shija Emanuel wa Hospital ya Rufaa ya Mjini Dodoma akipongezwa na Wafanyakazi wenzake mara baada ya kupewa Tuzo ya Cheti ya ufanyakazi Bora, kutokana na kufanya kazi yake ya kuzalisha kwa kufuata maadili

Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan akikagua mabanda ya kazi za uuguzi unahusisha wanawake na watoto kabla ya kuhitimisha kilele cha maadhimisho ya Siku ya wakunga Duniani iliyofanyika Kitaifa mjini Dodoma

 
Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan akipiga Makofi pamoja na Waziri wa Afya Ummy Mwalimu siku ya kilele cha maadhimisho ya Wakunga Duniani iliyofanyika Dodoma



Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Jordan Rugimbana akizungumza Jambo katika maadhimisho hayo
Rais Wa Chama cha Wakunga Nchini [TAMA] Feddy Anael Mwanga akizungumza katika maadhimisho hayo wakati alipokuwa akisoma Risala ya Wakumga Mbele ya Mgeni Rasmi Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan
Mtendaji Mkuu wa UNFPA Dkt, Hashina Begamu akiteta Jambo na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Jordan Rugimbana wakati wa Maadhimisho hayo
Waziri wa Afya Ummy Mwalimu akifurahia jambo wakati alipokuwa akiongea katika maadhimisho hayo




Picha ya Pamoja na watendaji wa Chama cha Wauguzi [TAMA]

Pamoja na waliopata Tuzo za vyeti

Mhadhili Msaidizi wa Chuo cha Wauguzi cha Kairuki cha Jijini Dar es laam Orivia Kroening- Roche akiwa ameshika Bango lilililoandikwa kuwa Uhai wa Mama na Mtoto Upo Mikononi mwa Mkunga huku picha ikionyesha mama akimfurahia mwanae baada ya kujifungua salama


NA JOHN BANDA, DODOMA
SERIKALI Imewataka wakuu wa Wilaya Nchini kuhakikisha kuwa zinajenga nyumba za watumisha wa kada ya Afya hasa maeneo ya vijijini na kipaumbele kitolewe kwa wakunga ambao mara nyingi ndiyo wanatoa huduma za Dharula kwa wanawake wajawazito na watoto.

Agizo hilo limetolewa na  Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan katika kilele cha maadhimisho ya siku ya wakunga Duniani ambayo yamehudhuriwa na wakunga toka mikoa mbalimbali nchini ambapo amesema kitendo cha kukaa mbali husababisha huduma kuwa Duni.

Aidha Makamu wa Rais amesema ili kubaini changamoto zinazosababisha vifo hivyo Mkunga wa zamu na msaidizi wake watatakiwa kutoa maelezo ya kina kuhusu kifo chochote kitakachotokea cha mama mjamzoto au mtoto wakati wa kujifungua

Awali Rais wa Chama cha wakunga nchini [TAMA] Feddy Anael Mwanga akisoma Risala ya chama hicho amesema kitendo cha wakunga kuishi umbali wa zaidi ya kilometa 2 inapotokea dharula ni vigumu kumpata

Post a Comment

Previous Post Next Post
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG