![]() |
| Afsa kilimo wa Wilaya ya Chemba mkoani Dodoma Chrisanti Sifunda akifafanua jambo wakati alipokuwa akiongea na wakalima wa Alizeti wilayani humo |
![]() |
| Mafunzo yakiendelea |
![]() |
| alizeti zikiwa shambani kabla ya kuvunwa |
![]() |
| wakulima wilayani Chemba wakijaza alizeti ilikwishavunwa kwenye mifuko kabla ya kuipeleka sokoni |
![]() |
| Mafunzo yakiendelea |
![]() |
![]() |
| mmoja wa wakulima hao akifurahia jambo wakati mafunzo hayo yakiendelea |
John Banda, Dodoma
WAKULIMA Nchini wameshauliwa kuvuna mazao
yaliyokomaa, kuyakausha na kuyahifadhi vizuri ili kuepukana na fangasi
anayezalisha vilusi vya sumu kuvu ambavyo ni hatari kwa afya ya binamu ikiwemo
vifo.
Usahauri huo umetolewa na Afsa kilimo wa Wilaya ya
Chemba mkoani Dodoma Chrisanti Sifunda wakati akiongea na wakulima wa zao la
alizeti wakati wa mafunzo ya kilimo, uvunaji na uhifadhi bora wa zao hilo
yaliyoratibiwa na Shirika linasindika mafuta ya alizeti, asali na Alovela la 3
Sisters Chini ya udhamini wa TECNO SAFE
Afsa huyo amewataka wakulima hao kuhakikisha
wanazingatia ushauri unaotolewa na wataraamu ikiwemo kuwa wepesi wa kuwafuata
na kuwaomba ushauri.
Aidha Sifunda ameyataja madhara yanasababishwa na
Sumu kuvu ikiwemo kuvimba tumbo, kuhara, kutapika, macho kuwa ya njano na kama
kiwango chake ni kikubwa husababisha vifo
Nae Mwakilishi wa Shirika linalosindika mazao ya
Alizeti, asali na alovela la 3 Sister la Mjini Dodoma Mariamu Majengo ameitaja sumu hiyo kuwa ni hatari kwa mwaka
2016 watu 17 walipoteza maisha katika baadhi ya vijiji wilayani Chemba baada ya
kula nyama ya ng’ombe ambaye alikuwa
kala pumba na alizeti iliyokuwa imeathiliwa na Sumu hiyo
Wakulima hawa John Molo na Moringe Kimosa wamesema
wamepata ufahamu wa kutosha kuhusu Sumu kuvu ambapo walikuwa wanaona dalili
zilizotajwa bila kujua na wakifahamu
kuwa sumu hiyo haifi hata ikipikwa na kutiwa chumvi
Tags
SUMU KUVU












