
Serikali imetangaza neema kwa wafanyabiashara wadogo wadogo wasio rasmi
wakiwamo mama lishe na baba lishe, ikiahidi kuwapa vitambulisho maalumu
vitavyosaidia kuwatambua rasmi.
Amesema vitambulisho hivyo vitawasaidia kutengewa maeneo maalumu ya kufanyia biashara.
Akiwasilisha mapendekezo ya bajeti kuu leo, Alhamisi kwa mwaka wa fedha
2017/18, Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Philip Mpango amesema hatua hiyo
inalenga kuwasaidia wafanyabiashara hao ili kukuza mitaji yao.