Waziri Mkuu wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa(Mb) akisalimiana na Kamishna
Jenerali wa Magereza, Dkt. Juma Malewa alipofanya ziara ya kikazi ya
kukagua maandalizi ya kufufua Kiwanda cha Sukari na Kilimo cha miwa
katika Gereza la Mbigiri Mkoani Morogoro Septemba 2, 2017. Jeshi la
Magereza kwa kushirikiana na Mifuko ya Jamii ya PPF na NSSF limeingia
ubia katika mradi huo wa uchumi wa viwanda chini ya Kampuni ya MKULAZI.
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa(Mb) akiangalia mbegu za miwa
kabla ya kuzipanda katika eneo la Shamba la miwa alipowasili Gereza
Mbigiri katika ziara ya kikazi ya kukagua maandalizi ya kufufua Kiwanda
cha Sukari na Kilimo cha miwa katika Gereza la Mbigiri Mkoani Morogoro
Septemba 2, 2017. Kulia ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera,
Bunge, Ajira na Watu wenye ulemavu) Mhe. Jenista Mhagama.
Shamba la miwa katika mradi wa
Kiwanda cha Sukari na Kilimo cha miwa – MKULAZI katika eneo la Gereza la
Mbigiri Mkoani Morogoro likiwa limestawi kama inavyoonekana katika
picha.
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa akitoa hotuba fupi kwa
Maafisa na askari wa Jeshi la Magereza Mkoani Morogoro, Watendaji wa
Kampuni ya MKULAZI pamoja na Wananchi wanaoishi jirani na Gereza Mbigiri
katika ziara ya kikazi ya kukagua maandalizi ya kufufua Kiwanda cha
Sukari na Kilimo cha miwa katika Gereza la Mbigiri Mkoani Morogoro
Septemba 2, 2017.
Kamishna Jenerali wa Magereza,
Dkt. Juma Malewa akitoa maelezo mafupi kwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim(hayupo pichani) namna Jeshi hilo
lilivyojipanga katika kuhakikisha kuwa ufufuaji wa Kiwanda cha Sukari na
Kilimo cha miwa katika Gereza la Mbigiri Mkoani Morogoro unakamilika
kama ilivyopangwa ambapo matarijio ni kuwa Kiwanda hicho kitakuwa na
uwezo wa kuzalisha sukari tani 50,000 kwa mwaka.
Baadhi ya Maafisa Waandamizi wa
Jeshi la Magereza pamoja na Wakuu wa Vyombo vya Ulinzi na Usalama wa
Mkoani Morogoro wakimsikiliza Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa alipofanya ziara ya kikazi ya kukagua
maandalizi ya kufufua Kiwanda cha Sukari na Kilimo cha miwa katika
Gereza la Mbigiri Mkoani Morogoro Septemba 2, 2017.
Mkurugenzi Mkuu wa NSSF Prof.
Godius Kyaharara akitoa maelezo mafupi kwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa alipofanya ziara ya kikazi ya
kukagua maandalizi ya kufufua Kiwanda cha Sukari na Kilimo cha miwa
katika Gereza la Mbigiri Mkoani Morogoro Septemba 2, 2017.
Kamishna Jenerali wa Magereza,
Dkt. Juma Malewa(kushoto) akiteta jambo na Waziri wa Viwanda, Biashara
na Uwekezaji, Mhe. Charles Mwijage(kulia) mara baada ya ziara ya Waziri
Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa ambapo amekagua maandalizi ya kufufua Kiwanda
cha Sukari na Kilimo cha miwa katika Gereza la Mbigiri Mkoani Morogoro
Septemba 2, 2017.
Mkurugenzi Mkuu wa PPF William
Erio akitoa neno la shukurani mbele ya Waziri Mkuu wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa alipofanya ziara ya kikazi ya
kukagua maandalizi ya kufufua Kiwanda cha Sukari na Kilimo cha miwa
katika Gereza la Mbigiri Mkoani Morogoro Septemba 2, 2017.
Ujenzi wa maghala ya kuhifadhia
sukari katika mradi wa Kiwanda cha Sukari cha MKULAZI kilichopo Gereza
Mbigiri ukiendelea katika hatua mbalimbali kama inavyoonekana katika
picha
Wataalam wazalendo ambao
wanajitolea katika ujenzi wa mradi wa Kiwanda cha Sukari – MKULAZI
Mbigiri wakitambulishwa mbele ya Waziri Mkuu, Mhe. Kassim
Majaliwa(hayupo pichani(Picha zote na Lucas Mboje wa Jeshi la Magereza).
Maafisa Waandamizi wa PPF na NSSF wakifuatilia kwa makini hotuba ya Waziri Mkuu, Mhe. Kassim Majaliwa(hayupo pichani).
Tags
Majaliwa Kassim