BANDA MEDIA BLOG

Klabu za Maadili kuanzia Shule za msingi – Waziri Jafo


1
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR-TAMISEMI) Mhe. Selemani Jafo akizungumza na washikriki wakati wa  uzinduzi wa maadhimisho ya siku ya maadili na haki za binadamu kitaifa   katika ukumbi wa mikutano Hazina Mjini Dodoma.
2
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR-TAMISEMI) Mhe. Selemani Jafo akizungumza na  Kamishna wa Maadili  Jaji Mstaafu  Harold Nsekela wakati wa  uzinduzi wa maadhimisho ya siku ya maadili na haki za binadamu kitaifa Mjini Dodoma.
3
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR-TAMISEMI) Mhe. Selemani Jafo akizindua rasmi maadhimisho ya siku ya Maadili na Haki za binadamu kitaifa   katika ukumbi wa mikutano Hazina Mjini Dodoma, leo

4
Baadhi ya washiriki waliohudhuria  katika uzinduzi wa maadhimisho ya siku ya maadili na haki za binadamu kitaifa katika ukumbi wa mikutano Hazina Mjini Dodoma.
5
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR-TAMISEMI) Mhe. Selemani Jafo akimkabidhi  kitabu cha muongozo wa  maadili na haki za binadamu   Katibu Mtendaji Tume ya haki za binadamu na Utawala  Bi. Mary Massay katika ukumbi wa mikutano Hazina Mjini Dodoma,leo
6
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR-TAMISEMI) Mhe. Selemani Jafo pamoja na  baadhi ya viongozi  kutoka katika taasisi mbalimbali za  haki za binadamu  na mwanafunzi wakionesha kitabu cha muongozo wa  Maadili na haki za binadamu  wakati wa Uzinduzi wa maadhimisho mjini Dodoma.
…………….
Nteghenjws Hosseah,OR-TAMISEMI.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR-TAMISEMI) Mhe. Selemani Jafo amewaagiza Wakurugenzi wote nchini kuhakikisha   wanasimamia uzishwaji wa klabu za maadili katika shule  zote za Msingi zilizopo katika maeneo yao.
Waziri Jafo pia amewataka Maafisa Elimu  Msingi na Sekondari Nchini    kutekeleza agizao hilo na kuwasilisha  ripoti  juu ya klabu ngapi za maadili zimeanzishwa katika maeneo ambayo wanayasimamia na taarifa iwasilishwe kabla ya  wake April 30,2018.
“ Ifikapo Tar. 30 mwezi wa  nne  mwakani kila afisa elimu  ahakikishe anandaa ripoti  ya Utekelezaji inayoonyesha katika Shule kadhaa  klabu ngapi za maadili zimeundwa  na hayo ni miongoni mwa mambo nitakayoyafanyia tathimni “
Waziri Jafo alitoa maagizo hayo mapema leo wakati wa Uzinduzi wa  maadhimisho ya Siku ya Maadili Kitaifa ambayo imekwenda sambamba na uzinduzi wa klabu kumi na tano  za maadili   uliambatana na uzinduzi wa mwongozo wa klabu hiyo uliofanyika  katika ukumbi wa Hazina  Mjini Dodoma.
Aliongeza kwa kuwataka maafisa elimu wote wahakikishe waanzisha klabu hizi, kuzilea na  na kuziwezesha  kwakuwa zoezi hili likifanywa kwa  umakini na kwa  ukubwa wake    litaweka    msingi imara katika kupata viongozi wenye uweledi na kusaidia kutengeneza vijana imara walioiva kimaadili  na kuondoa changamoto ya kukosekana kwa maadili katika jamii inayopelekea  uvutaji na utumiaji wa madawa ya kulevya, mimba na na ubadhilifu.
Wakati wa uzinduzi huo Waziri Jafo amewataka Viongozi na wananchi wote kuweka uzalendo mbele na uadilifu katika kutekeleza majukumu yetu yatakayoenda sambamba na kulinda rasilimali za Taifa hili.
“Bila uzalendo tutapoteza muelekeo katika Nchi yetu na rasilimali zote za Taifa hili zitapotea kwa kutumiwa na watu wachache na zaidi ya hapo vizazi vijavyo vitakosa kunufaika na rasilimali hizi ambazo ni muhimu kwa ustawi wao na ni haki yao ya msingi” alisema Waziri Jafo.
Katika uzinduzi huo Mhe. Jafo amezitaka Taasisi zote zinazoshughulikia  maadili kufanya kazi kwa uadilifu   kwa kutekeleza Mkakati dhidi  ya Rushwa na Mpango wa Utekelezaji wa Awamu ya Tatu uliozinduliwa rasmi na Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan   ili kuendeleza ajenda ya uzalendo na kuwafundisha wananchi kuwa wazalendo katika jamii.
Aidha amezishukuru ofisi mbalimbali zinazoratibu haki za binadamu  kwa kazi nzuri wanazozifanya   na  kutoa rai kwa  wadau wengine  hasa Watendaji wake Wakuu kujitafakari na kuona ni jinsi gani wanaweza kushiriki katika  kupambana na rushwa  na  kutoa elimu ya Uadilifu  katika utoaji wa huduma kwa wananchi.
Akizungumza wakati wa uzinduzi huo Kamishna wa Maadili Jaji (Mst) Harold Nsekela alisema Siku ya maadili inatokana na Siku ya Kimataifa ya kuzuia na kupambana na rushwa na maadimisho ya siku ya haki za Binadamu na kilele cha Siku hii  ktafanyika Dec 10 na kwa  kauli mbiu ya  inayobeba maadimisho haya ni “Uwajibika, piga  vita rushwa zingatia maadili ,haki za binadamu na utawala bora kuelekea uchumi wa kati”
Naye Mthibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali Prof. Mussa Assad amesema kuwa kupitia  mada zitakazowasilishwa katika uzinduzi  huo zitawapa  washiriki maarifa ya kuendelea kufanya kazi  kwa uweledi na kuongeza ubunifu  ili kuleta tija na maboresho  katika utendaji.
Tangu maadhimisho ya Siku ya Maadili kuanza yamesaidia kuongeza chachu  na kuamsha ari kwa wananchi kuunga mkono jitihada za Serikali ya Awamu ya Tano katika katika kulinda haki za Binadamu, kupiga vita rushwa na Ufisadi, uzembe na ubadhirifu wa mali za Umma.

Post a Comment

Previous Post Next Post
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG