Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano
wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa akiteta jambo na Kocha wa Timu wa ya
Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Venance Mwamoto wakati
alipokuwa akiwasalimia Wachezaji wa Timu ya Bunge la Tanzania na
Wachezaji wa Bunge la Burundi kabla ya kuanza kwa mechi baina ya timu
hizo Uwanja wa Taifa Jijini Dar es Salaam ambapo timu ya Bunge la
Tanzania ilishinda kwa mabao 3 – 1. Mechi hiyo lilichezwa ikiwa ni
sehemu ya Mashindano ya Kimichezo ya Mabunge ya Jumuiya ya Afrika
yalioanza mwishoni mwa wiki na yanatarajiwa kwisha tarehe 10 Desemba,
2017.
Mshambuliaji wa Timu ya Bunge
la Tanzania Mhe. Ridhiwan Kikwete akiwatoka Mabeki wa Timu ya Bunge la
Burundi wakati wa mechi baina ya timu hizo ikiwa ni sehemu ya Mashindano
ya Kimichezo ya Mabunge ya Jumuiya ya Afrika yalioanza mwishoni mwa
wiki na yanatarajiwa kwisha tarehe 10 Desemba, 2017 ambapo Timu ya Bunge
la Tanzania ilishinda kwa mabao 3-1.
Mshambuliaji wa Timu ya Bunge
la Tanzania Mhe. Ridhiwan Kikwete akipiga mpira kuelekea katika Lango
la Timu ya Bunge ya Burundi wakati wa mechi baina ya timu hizo ikiwa ni
sehemu ya Mashindano ya Kimichezo ya Mabunge ya Jumuiya ya Afrika
yalioanza mwishoni mwa wiki na yanatarajiwa kumalizika tarehe 10
Desemba, 2017 ambapo Timu ya Bunge la Tanzania ilishinda kwa mabao 3-1.
Kikosi
cha Timu ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika picha ya
Pamoja kabla ya kuanza kwa mechi yao na Timu ya Bunge la Burundi ambapo
walishinda 3-1
PICHA NA BUNGE
Tags
Bunge