Mwenyekiti wa Bunge la Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Mhe.Azzan Mussa Zungu akiongoza kikao cha
thelathini na saba cha mkutano wa kumi na moja Jijini Dodoma leo.
Naibu Waziri wa Kilimo Mhe.Dkt
Mary Mwanjelwa akieleza mikakati ya Serikali kuhakikisha kuwa zao la
korosho linaendea kuwanufaisha wakulima Bungeni Jijini Dodoma.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri
Mkuu Sera,Bunge,Kazi,Vijana,Ajira na wenye Ulemavu Mhe.Jenista Mhagama
akiteta jambo na Rais wa Umoja wa Vijana wa Bunge la Afrika na Mbunge wa
Handeni Vijijini Mhe.Mboni Mhita wakati wa kikao cha thelathini na
saba cha mkutano wa kumi na moja Jijini Dodoma leo.
Naibu Waziri wa Ardhi,Nyumba na
Maendeleo ya Makazi Mhe.Angeline Mabula akitolea ufafanuzi tofauti
iliyopo kati ya shule za Serikali na Binafsi na kusisitiza kwamba
mitaala ya kimataifa imeruhusiwa ili kukidhi mahitaji ya raia wa kigeni
wanaoishi nchini.
Waziri wa Fedha na Mipango
Mhe.Dkt.Philip Mpango akizungumza jambo na Mbunge wa Bunda Mjini wakati
wa kikao cha thelathini na saba cha mkutano wa kumi na moja Jijini
Dodoma leo.
Mbunge wa Viti Maalum
Mhe.Jacqueline Ngonyani akiomba ufafanuzi kwa Serikali kuhusu ulipaji wa
Mawakala wa pembejeo wakati wa kikao cha thelathini na saba cha mkutano
wa kumi na moja Jijini Dodoma leo.
Spika wa Bunge la Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Mhe.Job Ndugai akiwasalimie wabunge wakati wa
utambulisho wa Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe.Prof Ibrahim Juma (kushoto)
wakati wa kikao cha thelathini na saba cha mkutano wa kumi na moja
Jijini Dodoma leo.
Picha zote na Daudi Manongi, DODOMA
Tags
Bungeni