BANDA MEDIA BLOG

WAUMINI WA DINI YA KIISLAM WASHIRIKI KATIKA IBADA YA EID- EL- FITIR ILIYOANDALIWA NA KAMATI YA SHEREHE ZA KIISLAM JIJINI DODOMA

Waumini wa Dini ya Kiislam wakishiriki ibada ya Eid
Shekh wa Msikiti wa Nunge Ahmed Zuber akizungumza jambo wakati wa ibada ya Eid iliyofanyika katika uwanja wa jamhuri Jijini Dodoma 

Ibada ikiendelea [ PICHA ZOTE NA JOHN BANDA WA BANDA BLOG]




Waziri wa Tawala za mikoa na serikali za mitaa Suleiman Jaffo katikati akishiriki ibada ya Eid jijini Dodoma



Na John Banda, Dodoma

Kamati ya Sherehe za Kiislamu Jijini Dodoma imewataka waumini wa dini  hiyo kuacha mizozo ikiwemo kutengeneza vikundi vya mashindano badala yake wawe wamoja ili iwe rahisi kupata maendeleo 

Akizungumza katika Ibada ya Sala ya Eid – el – Fitr SHEKH wa msikiti wa Nunge Ahamed Zubery amesema Damu haiwezi kufuta damu
“bila umoja hatuwezi kuendelea hata kidogo tunayoyataka hatuwezi kuyapata tuondoleane mipaka tuweni wamoja kwa kuwa vikundi visivyokuwa na maana vinazidi hebu tuondoleane mizozo tusameheane kwa kuwa Damu haiwezi kufuta damu”, alisema

Aidha Sekh Zubery amewataka Waumini hao kuacha mashindano na badala yake wajiingize katika kutafuta Elimu ili kuondokana na manung’uniko ya kuonewa  kila wakati.

Kwa upande wake Ustaadh Omary akitoa mawadha katika ibada hiyo amesema imefika wakati ambao kila muislam jijini Dodoma kuwachukua watoto yatima na wanaoishi katika mazingira magumu ili kuishi nae njia ambayo itawasababishia Baraka
  

Post a Comment

Previous Post Next Post
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG
BANDA MEDIA BLOG